16 WANAODAIWA KUKWAPUA FEDHA ZA USHIRIKA WILAYANI HAI WAWEKWA NDANI KWA AMRI YA DC SABAYA

16 WANAODAIWA KUKWAPUA FEDHA ZA USHIRIKA WILAYANI HAI WAWEKWA NDANI KWA AMRI YA DC SABAYA - Hallo rafiki WORLD MAELEZO LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa 16 WANAODAIWA KUKWAPUA FEDHA ZA USHIRIKA WILAYANI HAI WAWEKWA NDANI KWA AMRI YA DC SABAYA, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala biashara, makala general, makala hobby, makala karibuni info, makala michezo, makala siasa, makala utamaduni, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : 16 WANAODAIWA KUKWAPUA FEDHA ZA USHIRIKA WILAYANI HAI WAWEKWA NDANI KWA AMRI YA DC SABAYA
kiungo : 16 WANAODAIWA KUKWAPUA FEDHA ZA USHIRIKA WILAYANI HAI WAWEKWA NDANI KWA AMRI YA DC SABAYA

soma pia


16 WANAODAIWA KUKWAPUA FEDHA ZA USHIRIKA WILAYANI HAI WAWEKWA NDANI KWA AMRI YA DC SABAYA

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii,
Kanda ya Kaskazini.
WATU 16 wakiwemo viongozi wa Bodi ya Ushirika wa Umoja wa watumia maji katika kijiji cha Mijongweni (UWAMI) wanashikiliwa na Jeshi la  Polisi kwa amri ya mkuu wa wilaya ya Hai,Lengai Ole Sabaya  wakituhumiwa kuhusika na ubadhilifu wa fedha za mradi zaidi ya Sh Mil 200.
Mbali na Viongozi wa Bodi ya ushirika huo wakiongozwa na Mwenyekiti wake ,Nuru Ndoma pia wamo baadhi ya wajumbe wa serikali ya kijiji, Viongozi wa kamati ya mpito ya kusimamia mradi huo ikiongozwa na Alex Mkwizu.
Kukamatwa kwa Viongozi hao kunatokana na taarifa ya uchunguzi uliofanywa na kamati iliyoundwa na  Mkuu huyo wa wilaya kuchunguza madai ya ubadhilifu wa fedha baada ya kukataa taarifa yaawali ya  kamati kama hiyo iliyoundwa na aliyekuwa mkuu wa wilaya hiyo Gelasius Byakanwa.
Tuhuma zinazowakabili watu hao zimetajwa kuwa ni pamoja na kuuzwa kinyemela kwa Mashine ya kulimia (Power tiller ) aina ya Kubota iliyotolewa na Wizara ya Kilimo kwa kijiji cha Mijongweni ambayo inatajwa kuuzwa kwa mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la Yusuph Losindilo.
Baadhi ya viongozi hao pia wanatajwa kutakatisha fedha za malipo ya ukodishwaji wa mashine ya kuvunia Mpunga kwa kuziingiza katika akaunti ya kijiji na kasha kuzitoa wakati huo huo na kuzipangia matumizi yasiyokuwa na maelezo ya kutoshereza.
Aidha watu hao pia wanadaiwa kuuza baadhi ya vipuri vya Mashine hizo na baadae kuonesha kuwa wamenunua vipuri kwa ajili ya matengenezo ya mashine hizo huku ikionyesha vipuri vinavyodaiwa kununuliwa ni vile vilivyoletwa pamoja na mashine.
Mkuu wa wilaya ya Hai,Lengai Ole Sabaya akizungumza wakati wa mkutano wa utoaji wa taarifa ya uchunguzi wa kamati iliyoundwa na mkuu huyo kuchunguza ubadhilifu wa fedha za Ushirika wa watumia maji katika kijiji cha Mijongweni.
Mkuu wa wilaya ya Hai,Lengai Ole Sabaya akiwahoji baadhi ya wajumbe wa serikali ya kijiji cha Mijongweni kuhusiana na ubadhilifu uliofanyika katika Ushirika huo.
Moja ya Mashine hizo ikiwa tayari imeharibika baada ya kuondolewa Roller inayotumika kwa ajili ya kutembelea.
Mashine mpya ya Ushirika huo ambayo haijaanza kutumika bado.
Baadhi ya watuhumiwa wa ubadhilifu wa fedha za Mradi wa Ushirika huo wakiwa kwenye gari la Polisi mara baada ya kukamatwa wakiwa eneo la mkutano.


Hivyo makala 16 WANAODAIWA KUKWAPUA FEDHA ZA USHIRIKA WILAYANI HAI WAWEKWA NDANI KWA AMRI YA DC SABAYA

yaani makala yote 16 WANAODAIWA KUKWAPUA FEDHA ZA USHIRIKA WILAYANI HAI WAWEKWA NDANI KWA AMRI YA DC SABAYA Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala 16 WANAODAIWA KUKWAPUA FEDHA ZA USHIRIKA WILAYANI HAI WAWEKWA NDANI KWA AMRI YA DC SABAYA mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/08/16-wanaodaiwa-kukwapua-fedha-za.html

Subscribe to receive free email updates:

0 Response to "16 WANAODAIWA KUKWAPUA FEDHA ZA USHIRIKA WILAYANI HAI WAWEKWA NDANI KWA AMRI YA DC SABAYA"

Post a Comment