title : TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI (NEC) YATANGAZA UCHAGUZI MDOGO JIMBO MOJA NA KATA 79
kiungo : TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI (NEC) YATANGAZA UCHAGUZI MDOGO JIMBO MOJA NA KATA 79
TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI (NEC) YATANGAZA UCHAGUZI MDOGO JIMBO MOJA NA KATA 79
TumeyaTaifayaUchaguzi (NEC) itafanya uchaguzi mdogo kwenye Jimbo la Buyungu, Mkoani Kigoma na kwenye Kata 79 za Tanzania Bara, Mwenyekiti wa NEC, Jaji (R), Semistocles Kaijage amesema.
Akizungumza Jijini Dar es Salaam jana, Jaji Kaijage amesema uchaguzi huo utafanyika tarehe 12 mwezi ujao (Agosti) na fomu za uteuzi wa wagombea zitatolewa kuanzia tarehe 8 hadi 14 mwenzi huu (Julai).
"Uteuzi wa Wagombea utafanyika tarehe 14 Julai, mwaka huu. Kampeni za Uchaguzi zitafanyika kati ya tarehe 15 Julai, hadi tarehe 11 Agosti, mwaka huu na siku ya uchaguzi itakuwa ni tarehe 12 Agosti mwaka huu,” alisema.
Jaji Kaijage amebainisha kwamba Tume imetangaza uwepo wa nafasi wazi ya Ubunge kwenye Jimbo hilo la Buyungu baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Ndugu Job Ndugai.
“Tumeilipokea barua kutoka kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye kwa kuzingatia kifungu cha 37(3) cha Sheria ya Taifaya Uchaguzi, Suraya 343, aliitarifu Tume uwepo wa nafasi wazi ya Mbunge wa Jimbo la Buyungu katika Halmashauri ya Kakonko Mkoani Kigoma kufuatia kufariki kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo Mheshimiwa Kasuku Samson Bilago,” alisema.
Kwa upande wa nafasi wazi za Udiwani, Mwenyekiti huyo alisema Tumeilipokea taarifa kutoka kwa waziri mwenye dhamana akiitaarifu juu ya uwepo wa nafasi hizo na taratibu za uchaguzi mdogo zikaanza mara moja.
“Tumeimepokea Taarifa kutoka kwa Waziri mwenye dhamana na Serikali za Mitaa ambaye kwa kutumia mamlaka aliyopewa chini ya Kifungu cha 13(1) cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali zaMitaa, Sura ya 292, aliitarifu Tume uwepo wa nafasi wazi za Madiwani katika Kata 79 za Tanzania Bara,” alisema.
Akitoa wito kwa vyama vya siasa, Jaji Kaijage amesema “tunapenda kuvikumbusha Vyama vya Siasa na wadau wote wa uchaguzi kuzingatia Sheria, Kanuni, Maadiliya Uchaguzi, Taratibu, Miongozo na maelekezo yote wakati wa kipindi cha Uchaguzi mdogo”.
JajiKaijagealisemakwambauchaguzihuomdogoutafanyikandaniyaHalmashauri 43zilizopokwenyeMikoa 24ya Tanzania Bara.
Mikoa hiyo ni pamoja na, Kigoma, Arusha, Dar es Salaam, Dodoma, Iringa, Kagera, Katavi, Kilimanjaro, Lindi, Manyara, Mara, Mbeya, Mtwara, Morogoro, Mwanza, Njombe, Rukwa, Ruvuma, Shinyanga, Simiyu, Singida, Songwe, TaboranaTanga.
Halmashauri hizo ni pamoja na Moshi, Ruangwa, Mbulu, Hanang, Babati, Serengeti, Tarime, Kyela, Mtwara, Newala, Kilombero, Kilosa, Kwimba, Makete, Wanging’ombe, Kalambo, Songea, Msalala, Meatu, Singida, Songwe, Tunduma, Tabora, Nzega, UrambonaTanga.
Halmashauri nyingine ni pamoja na Karatu, Longido, Arusha, Ngorongoro, Monduli, Meru, Ubungo, Kondoa, Mpwapwa, Chamwino, Iringa, Kyerwa, Misenyi, Muleba, Nsimbo, KasulunaSame.
Hivyo makala TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI (NEC) YATANGAZA UCHAGUZI MDOGO JIMBO MOJA NA KATA 79
yaani makala yote TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI (NEC) YATANGAZA UCHAGUZI MDOGO JIMBO MOJA NA KATA 79 Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI (NEC) YATANGAZA UCHAGUZI MDOGO JIMBO MOJA NA KATA 79 mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/07/tume-ya-taifa-ya-uchaguzi-nec-yatangaza.html
0 Response to "TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI (NEC) YATANGAZA UCHAGUZI MDOGO JIMBO MOJA NA KATA 79"
Post a Comment