UVCCM KIGOMA WAHAMASISHWA KUBUNI MIRADI YA MAENDELEO

UVCCM KIGOMA WAHAMASISHWA KUBUNI MIRADI YA MAENDELEO - Hallo rafiki WORLD MAELEZO LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa UVCCM KIGOMA WAHAMASISHWA KUBUNI MIRADI YA MAENDELEO, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala biashara, makala general, makala hobby, makala karibuni info, makala michezo, makala siasa, makala utamaduni, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : UVCCM KIGOMA WAHAMASISHWA KUBUNI MIRADI YA MAENDELEO
kiungo : UVCCM KIGOMA WAHAMASISHWA KUBUNI MIRADI YA MAENDELEO

soma pia


UVCCM KIGOMA WAHAMASISHWA KUBUNI MIRADI YA MAENDELEO

Na Rhoda Ezekiel, Kigoma

UMOJA wa Vijana wa Chama Cha Mapindizi(UVCCM), Mkoa wa Kigoma wametakiwa kubuni miradi ya kimaendeleo kwa lengo la kupunguza kuomba misaada na kubwa zaidi kujiimarisha kwenye uchumi ili kuunga mkono kauli mbiu ya Uchumi wa viwanda.

Mwito huo ulitolewa jana na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa MNEC, Kilumbe Ngenda aliyekuwa mgeni rasmi, Katika Baraza la Vijana wa UVCCM Mkoa wa Kigoma katika uchaguzi wa wajumbe watatu wa kamati ya utekelezaji ya UVCCM Mkoa na kumthibitisha Katibu wa uhamasishaji na chipukizi.

Ambapo aliwataka vijana hao kubuni miradi na kuendeleza miradi waliyonayo kama jumuiya nyingine zinavyo fanya na kuwataka kuwa na miradi yao binafsi ili kupunguza tabia ya kutembea na mabakuli kuomba.
Pia ameahdi kutoa mifuko 50 ya saruji ili wabuni mradi ikiwa ni pamoja na kuanzisha viwanda na kuiboresha nyumba ya wageni ambayo ipo chini ya vijana hao iliyopo Manispaa ya Kigoma Ujiji.Aidha Mbunge kupitia Vijana mkoa huo, Zainabu Katimba, amesema yeye kama kiongozi wa vijana ameamua kutoa Sh.milioni saba kwaajili ya kuwasaidia vijana Wilaya zote kuanzisha miradi ikiwamo miradi itakayohusisha viwanda.

Pia ametoa cherehani tatu kwa kikundi cha vijana wajasiriamali cha Mwandiga na kuwataka waendelee na jitihada za kuhakikisha vijana wote wanakuwa na shughuli za kufanya na kila Wilaya wabuni miradi."Sisi viongozi tutahakikisha tunawasaidia kuwawezesha ili kuanzisha vikundi vya ujasiriamali na kuanzisha viwanda ambavyo vitatoa ajira kwa vijana wengi,"amesema.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa Wa Kigoma, Silvia Sigura amesema wao wamejipanga kufanya siasa za uchumi na si siasa za maneno na kwa kudhihirisha hilo wmeanza harambee kwa vijana katika baraza lililofanyika na kufanikiwa kuchangisha mifuko ya saruji 130 ili kuanza kujenga vibanda 12 katika kiwanja chao.

Amesema kwa michango walioipata watahakikisha wanaanzisha miradi kwa kila wilaya na kutoa elimu ya ujasiriamali kwa vijana ili wajiajiri katika masuala ya ujasiriamali.


Hivyo makala UVCCM KIGOMA WAHAMASISHWA KUBUNI MIRADI YA MAENDELEO

yaani makala yote UVCCM KIGOMA WAHAMASISHWA KUBUNI MIRADI YA MAENDELEO Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala UVCCM KIGOMA WAHAMASISHWA KUBUNI MIRADI YA MAENDELEO mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/03/uvccm-kigoma-wahamasishwa-kubuni-miradi.html

Subscribe to receive free email updates:

0 Response to "UVCCM KIGOMA WAHAMASISHWA KUBUNI MIRADI YA MAENDELEO"

Post a Comment