title : RC TABORA: WAKANDARASI WA KITANZANIA HAKIKISHENI MIRADI YENU INAKUWA YA KIWANGO CHA JUU
kiungo : RC TABORA: WAKANDARASI WA KITANZANIA HAKIKISHENI MIRADI YENU INAKUWA YA KIWANGO CHA JUU
RC TABORA: WAKANDARASI WA KITANZANIA HAKIKISHENI MIRADI YENU INAKUWA YA KIWANGO CHA JUU
Na Tiganya Vincent
WAKANDARASI Kitanzania wametakiwa kuzingatia ubora, viwango vya kazi zao ili waweze kuaminika kwa Serikali na hivyo kupata fursa kubwa ya kupewa miradi mipya inayotarajiwa kujengwa hapa nchini.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri wakati alipokutana na ujumbe wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi(CRB)
Alisema ujenzi wa miradi chini ya kiwango na ambayo haidumu kwa muda mrefu kutawasababisha kutopewa kipaumbele pindi miradi inapokuwa ikitangazwa na badala yake miradi hiyo kutekelezw na wakandarasi wa kigeni.
Mwanri alisema ni vema wajenga tabia ya kushirikiana katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ili waweze kuwa na nguvu kubwa na vifaa vingi ambavyo ndivyo vitawasaidia kuikamisha kwa wakati na kwa kiwango bora kinachotakiwa.
Alisema matokeo mazuri ya utekelezaji wa miradi yataifanya Serikali kutoa kipaumbele kwa Kampuni za Watanzania katika miradi ya ujenzi , jambo ambalo litawasaidia kujiimarisha zaidi.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri(kulia) akiagana jana na Meneja wa Wakala wa Barabarani Tanzania(TANROADS) Mkoani humo, Damian Ndabalinze (kushoto) mara baada ya mazungumzo yaliyolenga kujua hali ya ukarabati wa barabara zilizoharibiwa na mvua iliyonyesha hivi karibuni na kusababisha kukatika kwa mawasilano katika njia mbalimbali.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri(kulia) akitoa maagizo jana kwa Mfanyakazi katika Kitalu cha Miche ya Miti mbalimbali cha Manispaa ya Tabora, Mariam Christopher(kushoto) na Meneja wa Wakala wa Mistu Tanzania (TFS) Manispaa ya Tabora Bakilana Mashauri (katikati) kuhusu kuotesha miti maji mingi kwa ajili ya kupanda katika maeneo mbalimbali katika Manispaa hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri(kulia) akitoa maagizo jana kwa Meneja wa Wakala wa Mistu Tanzania (TFS) Manispaa ya Tabora, Bakilana Mashauri (kulia) kuhusu kuotesha miti maji mingi kwa ajili ya kupanda katika maeneo mbalimbali katika Manispaa hiyo.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Hivyo makala RC TABORA: WAKANDARASI WA KITANZANIA HAKIKISHENI MIRADI YENU INAKUWA YA KIWANGO CHA JUU
yaani makala yote RC TABORA: WAKANDARASI WA KITANZANIA HAKIKISHENI MIRADI YENU INAKUWA YA KIWANGO CHA JUU Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala RC TABORA: WAKANDARASI WA KITANZANIA HAKIKISHENI MIRADI YENU INAKUWA YA KIWANGO CHA JUU mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/03/rc-tabora-wakandarasi-wa-kitanzania.html
0 Response to "RC TABORA: WAKANDARASI WA KITANZANIA HAKIKISHENI MIRADI YENU INAKUWA YA KIWANGO CHA JUU"
Post a Comment