title : MAKAMU WA RAIS AFANYA ZIARA WILAYANI MUFINDI
kiungo : MAKAMU WA RAIS AFANYA ZIARA WILAYANI MUFINDI
MAKAMU WA RAIS AFANYA ZIARA WILAYANI MUFINDI
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakazi wa Mafinga waliojitokeza kwenye uwekaji wa jiwe la msingi la upanuzi wa kituo cha Afya cha Ihongole. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan
amesema Serikali inajitahidi kujenga na kutanua vituo vya Afya ikiwa na
lengo la kupunguza msongamano kwenye hospitali za Wilaya.
Makamu
wa Rais ameyasema hayo leo wakati wa kuweka jiwe la msingi la upanuzi
wa kituo cha Afya Ihongole kilichopo mjini Mafinga.
Makamu
wa Rais ambaye yupo kwenye ziara ya kuhamasisha shughuli za kimaendeleo
mkoani Iringa ambapo leo alitembele wilaya ya Mufindi na kuweka mawe ya
msingi katika miradi miwili ikiwa mmoja ni wa kujenga maabara ya kisasa
na madarasa na kidato cha tano na cha sita katika Sekondari ya Mgololo
na upanuzi wa kituo cha Afya cha Ihongole kilichopo Mafinga.
Akiwahutubia
wananchi waliojitokeza kushuhudia uwekaji wa jiwe la msingi la Upanuzi
wa kituo cha Afya Ihongole , Makamu wa Rais alisema katika kila kituo
cha afya kinachopanuliwa ama kujengwa Serikali imezingatia huduma za
mama na mtoto ili kupunguza vifo vya akinamama na watoto, kuborsha
huduma za upasuaji .
Serikali
imetoa shilingi milioni 500 kwa ajili ya upanuzi wa kituo hicho na
kutumia mafundi wa kawaida kujenga ilikuweza kusaidia kutoa ajira kwa
vijana zaidi wa eneo husika.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akiweka jiwe la msingi la upanuzi wa ujenzi wa kituo cha afya Ihongole Mafinga, kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Iringa Bi. Amina Masenza.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisoma maneno yalioandikwa kwenye jiwe la msingi la ujenzi wa maabara na madarasa ya kidato cha tano na sita katika shule ya sekondari ya Mgololo, Mufindi mkoani Iringa mara baada ya kulifungua ,pembeni yake ni Mwenyekiti wa Makampuni ya Rai wanaomiliki kiwanda cha Mufindi Paper Mills Bw. Jaswant S. Rai na kulia ni Mkuu wa mkoa wa Iringa Bi. Amina Masenza.
Hivyo makala MAKAMU WA RAIS AFANYA ZIARA WILAYANI MUFINDI
yaani makala yote MAKAMU WA RAIS AFANYA ZIARA WILAYANI MUFINDI Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala MAKAMU WA RAIS AFANYA ZIARA WILAYANI MUFINDI mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/02/makamu-wa-rais-afanya-ziara-wilayani_12.html
0 Response to "MAKAMU WA RAIS AFANYA ZIARA WILAYANI MUFINDI"
Post a Comment