title : WAWEKEZAJI SEKTA YA UHIFADHI WAKABILIWA NA CHANGAMOTO LUKUKI
kiungo : WAWEKEZAJI SEKTA YA UHIFADHI WAKABILIWA NA CHANGAMOTO LUKUKI
WAWEKEZAJI SEKTA YA UHIFADHI WAKABILIWA NA CHANGAMOTO LUKUKI
Wawekezaji nchini katika sekta ya utalii na uhifadhi bado wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo uvamizi wa maeneo ,migogoro ya ardhi na kutokuwepo kwa eneo la malisho, hali ambayo imekuwa ikikwamisha jitihada za uwekezaji katika sekta hiyo.
Ambapo wanakijiji wengi bado wanaishi katika maisha ya asilia hali ambayo inapekea kuharibu uhifadhi kwani wamekuwa wakilisha mifugo yao bila kujali kuwa huo ni uharibifu wa mazingira ya utalii nchini .
Hayo yameelezwa leo na Meneja Mkuu kutoka Dhana Investment Company David Laizer katika mafunzo yaliyoandaliwa na Shirikisho la Vyama Vya Utalii Tanzania (TCT) kwa kushirikiana na Chuo Kikuu Cha Dar Es Salaam kitengo cha sera na utetezi (CPRA) kimefanya mafunzo ya siku mbili ya kuweka na kuendesha mfumo wa mdahalo (PPD) utakaowawezesha jamii katika ngazi za chini kuweza kuendesha mijadala ya maendeleo kati yao na wawekezaji na kushughulikia changamoto zinazowakabili katika maeneo yao ya uwekezaji. yaliyofanyika Mkoani Arusha.
Aidha alisema kuwa kuna haja ya Serikali kuingilia kati katika migogoro hiyo ili kuweza kuwawekea mazingira rafiki kwa wawekezaji uhifadhi na utalii nchini.Kwa upande wake Msemaji wa jumuiya ya Burunge Ramadhani Ismail amesema kuwa Serikali iangalie miundombinu ya uhifadhi ili kuziwezesha hifadhi na jumuiya zake ziweze kujiendesha na wananchi wapate manufaa kupitia jumuiya hizo.
Kwa upande wake mtoa mafunzo wa utetezi kutoka chuo kikuu ,idara ya masoko utafiti utetezi Dkt.Goodluck Urasa amesema kuwa wanatoa mafunzo hayo ili kuweza kuwasaidia jumuiya hizo kujengewa uwezo ili kuwewezesha jumuiya hizo ili kunufauika na uhifadhi.
Mafunzo hayo yatawasaidia katika kujenga jumuiya za uhufadhi zilizo na manuifaa bora.Kwa Upande wake mchambuzi wa sera kutoka tct Mosses ngereza alisema kuwa wameandaa mafunzo hayo ili kuwapa
mafunzo ya siku mbili ili kuweka na kuendesha mfumo wa mdahalo (PPD) utakaowawezesha jamii katika ngazi za chini kuweza kuendesha mijadala ya maendeleo kati yao na wawekezaji na kushughulikia changamoto zinazowakabili katika maeneo yao ya uwekezaji.
Aliongeza kuwa mbali na jitihada za kuwapa mafunzo lakini bado kuna changamoto yakutokuwa na wawekezaji wakutosjha katika sekta hiyo.
Hivyo makala WAWEKEZAJI SEKTA YA UHIFADHI WAKABILIWA NA CHANGAMOTO LUKUKI
yaani makala yote WAWEKEZAJI SEKTA YA UHIFADHI WAKABILIWA NA CHANGAMOTO LUKUKI Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala WAWEKEZAJI SEKTA YA UHIFADHI WAKABILIWA NA CHANGAMOTO LUKUKI mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/12/wawekezaji-sekta-ya-uhifadhi-wakabiliwa.html
0 Response to "WAWEKEZAJI SEKTA YA UHIFADHI WAKABILIWA NA CHANGAMOTO LUKUKI"
Post a Comment