title : Tundu Lissu Kufanyiwa Upasuaji wa 15
kiungo : Tundu Lissu Kufanyiwa Upasuaji wa 15
Tundu Lissu Kufanyiwa Upasuaji wa 15
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema kuwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu amefanywa upasuaji mara 14 na ataendelea kufanyiwa upasuaji mwingine wa 15 ndani ya wiki mbili zijazo.
Mbowe amesema hayo jana kwenye mazishi ya marehemu Philip Gekul, baba mzazi wa Mbunge wa Babati Mjini, Pauline Gekul yaliyofanyika kata ya Dareda.
Alisema hali ya Lissu inaendelea kuimarika lakini aliumizwa sana kama walivyokuwa wanaeleza mara zote lakini na jambo la kumshukuru Mungu kwamba ameendelea kuimarika.
"Ameendelea kupata afya, akili zake ni timamu, madaktari kule wanafanya kazi kubwa kwelikweli kuendelea kumuudumia na ni matumaini yetu kuwa baada ya muda Mungu atamrejesha katika wajibu wake wa kulitumikia Taifa,"
Mbowe alizungumza hayo baada ya kueleza kuwa alitokea Nairobi kuangalia afya ya mbunge huyo ambaye alipigwa risasi Septemba 7 mwaka huu akiwa nyumbani kwake mjini Dodoma.
Hivyo makala Tundu Lissu Kufanyiwa Upasuaji wa 15
yaani makala yote Tundu Lissu Kufanyiwa Upasuaji wa 15 Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala Tundu Lissu Kufanyiwa Upasuaji wa 15 mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/10/tundu-lissu-kufanyiwa-upasuaji-wa-15_8.html
0 Response to "Tundu Lissu Kufanyiwa Upasuaji wa 15"
Post a Comment