title : RC Rukwa aahidi kuimarisha utendaji kazi wa watumishi wa Rukwa katika Sekta zote
kiungo : RC Rukwa aahidi kuimarisha utendaji kazi wa watumishi wa Rukwa katika Sekta zote
RC Rukwa aahidi kuimarisha utendaji kazi wa watumishi wa Rukwa katika Sekta zote
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joackim Wangabo amewatahadharisha watumishi kutobweteka baada ya aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen kustaafu na kumkabidhi yeye kijiti cha utekelezaji wa shughuli za maendeleo ya mkoa.
Amesema kuwa hatomwangusha Rais Dk. John Pombe Magufuli kwa kumuamini na kumkabidhi madaraka hayo na kuahidi kuwa ataimarisha elimu inayoonekana bado ipo chini kwa ufaulu lakini pia kuendeleza kasi ya uzalishaji katika kilimo.
“Baada ya kusoma kabrasha hili la kukabidhiana ofisi kuna mambo mengi ya kuyazingatia ikiwemo, elimu, kilimo, ulinzi na usalama, utunzaji wa mazingira, uvuvi na uwekezaji katika viwanda. Hasa katika elimu maana mimba ni nyingi, kuna upungufu wa madawati, upungufu wa vyumba vya madarasa lakini pia kiwango cha ufaulu hakijafikia kile kilichopo katika ilani ya Chama cha Mapinduzi ambayo ni asilimia 80 kwa darasa la saba,” Alisisitiza.
Mh. Wangabo ameyasema hayo katika makabidhiano ya ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa mapema leo hii tarehe 31/10/2017 katika ukumbi wa ofisi hiyo, jambo lililoshuhudiwa na watumishi wa sekretariet ya Mkoa pamoja na baadha ya Halamashauri.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joackim Leonard Wangabo (kushoto) na Mh. Zelote Stephen (Waliokaa) katika picha ya pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa, Wakuu wa Wilaya pamoja na baadhi ya Wakurugenzi wa Halmashauri na Mwenyekiti wa CCM Mkoa.
Mkuu nwa Mkoa wa Rukwa, Mh. Joachim Leonard Wangabo akisalimiana na Meneja wa PS3 Mkoa wa Rukwa Bi. Rose wakati wa kumkaribisha Mh. Wangabo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa tayari kwaajili ya Kuanza kazi.
Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Kamishna Mstaafu Zelote Stephen (kushoto) akimkabidhi nyaraka za ofisi Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joackim Wangabo. katika makabidhiano ya ofisi hiyo yaliyofanyika katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa.
Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Kamishna Mstaafu Zelote Stephen (kushoto) akisaini nyaraka za ofisi Mkuu wa Mkoa kwaajili ya Kumkabidhi ofisi hiyo Rukwa Mh. Joackim Wangabo.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Hivyo makala RC Rukwa aahidi kuimarisha utendaji kazi wa watumishi wa Rukwa katika Sekta zote
yaani makala yote RC Rukwa aahidi kuimarisha utendaji kazi wa watumishi wa Rukwa katika Sekta zote Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala RC Rukwa aahidi kuimarisha utendaji kazi wa watumishi wa Rukwa katika Sekta zote mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/10/rc-rukwa-aahidi-kuimarisha-utendaji.html
0 Response to "RC Rukwa aahidi kuimarisha utendaji kazi wa watumishi wa Rukwa katika Sekta zote"
Post a Comment