title : Mkuu wa Wilaya ya Monduli Mhe. Iddi Hassan Kimanta aongoza mazishi ya watoto watatu waliofariki dunia baada ya kulipukiwa na bomu
kiungo : Mkuu wa Wilaya ya Monduli Mhe. Iddi Hassan Kimanta aongoza mazishi ya watoto watatu waliofariki dunia baada ya kulipukiwa na bomu
Mkuu wa Wilaya ya Monduli Mhe. Iddi Hassan Kimanta aongoza mazishi ya watoto watatu waliofariki dunia baada ya kulipukiwa na bomu
Mkuu wa Wilaya ya Monduli Mhe. Iddi Hassan Kimanta leo ameongoza waombolezaji katika mazishi ya watoto watatu waliofariki dunia kwa mlipuko wa bomu kwenye eneo la mazoezi ya kijeshi wilayani Monduli, mkoani Arusha.
Marehemu hao - Johnson Daniel, Lendisi Saitabau na Samweli Nyangusi -walifariki dunia Ijumaa iliyopita katika Kijiji cha Nafco kilichopo Kata ya Loksale walipokuwa wakichunga ng'ombe. Inasemekana walilipukiwa na bomu walipokuwa wakilichezea wakidhani ni mpira.
Mazishi hayo yamefanyika katika Kijiji cha Nafco kilichopo Kata ya Loksale wilayani Monduli, Mkoa wa Arusha baada ya shughuli ya kuaga miili hiyo katika Hospitali ya Wilaya ya Monduli.
Wanafunzi wa shule ya msingi Nafcon wakiwa wamebeba majeneza yenye miili ya wanafunzi wenzao mara baada ya kuwasili nyumbani kutokea hospitali ya wilaya ya Monduli kabla ya mazishi katika Kijiji cha Nafco kilichopo Kata ya Loksale wilayani Monduli, Mkoa wa Arusha
Mkuu wa Wilaya ya Monduli Mhe. Iddi Hassan Kimanta akitoa rambirambi za serikali kwenye mazishi hayo katika Kijiji cha Nafco kilichopo Kata ya Loksale wilayani Monduli, Mkoa wa Arusha baada ya shughuli ya kuaga miili hiyo katika Hospitali ya Wilaya ya Monduli.
Ibada ya mazishi katika Kijiji cha Nafco kilichopo Kata ya Loksale wilayani Monduli, Mkoa wa Arusha
Sehemu ya waombolezaji kwenye mazishi hayoAskari wa JWTZ wakiwa wamebeba moja ya majeneza ya marehemu hao wakielekea makaburini kwa mazishi.
Hivyo makala Mkuu wa Wilaya ya Monduli Mhe. Iddi Hassan Kimanta aongoza mazishi ya watoto watatu waliofariki dunia baada ya kulipukiwa na bomu
yaani makala yote Mkuu wa Wilaya ya Monduli Mhe. Iddi Hassan Kimanta aongoza mazishi ya watoto watatu waliofariki dunia baada ya kulipukiwa na bomu Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala Mkuu wa Wilaya ya Monduli Mhe. Iddi Hassan Kimanta aongoza mazishi ya watoto watatu waliofariki dunia baada ya kulipukiwa na bomu mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/09/mkuu-wa-wilaya-ya-monduli-mhe-iddi.html
0 Response to "Mkuu wa Wilaya ya Monduli Mhe. Iddi Hassan Kimanta aongoza mazishi ya watoto watatu waliofariki dunia baada ya kulipukiwa na bomu"
Post a Comment