title : MAKOCHA VIJANA, WANAVYOFUNGUA AKILI ZA WAPENZI WA SOKA DUNIANI.
kiungo : MAKOCHA VIJANA, WANAVYOFUNGUA AKILI ZA WAPENZI WA SOKA DUNIANI.
MAKOCHA VIJANA, WANAVYOFUNGUA AKILI ZA WAPENZI WA SOKA DUNIANI.
Na. Honorius Mpangala.
Mwalimu ni fani pana ambayo imekuwa na majina tofauti mengi ambayo hutumika katika kitendo cha kufundisha.Licha ya kuwa kama jina la fani ya kuhawilisha maarifa toka kwa anayejua kwenda kwa asiyejua. Ila yapo majina mengi katika nyanja nyingi ambayo hutumika katika matendo hayo ya kuhawilisha maarifa.
Wako walimu wa mambo mbalimbali,pia kwavile wafanyao kazi hizo ni binadamu basi changamoto hutoke pia.
Katika mchezo wa soka kuna kocha ambaye hufanya kazi hiyo ya kufundisha wachezaji. Kwa miaka mingi fani hii ya ualimu wa soka ilichukuliwa kama fani ambayo wanaoweza kuitenda vyema ni wale waliocheza soka kwa madaraja ya Juu.
Lakini kwa kadiri miaka ilivyoweza kusogea mapinduzi ya dhana hiyo yalianza kutoweka taratibu baada ya kuona wako makocha ambao wanafanya vyema pasipo hata kucheza madaraja ya juu katika soka. Wako makocha ambao wametoa mafanikio kwa vilabu vikubwa wakati wao wamecheza katika madaraja ya chini.
Katika ulimwengu wa soka imekuja kuonekana,kucheza soka ni kama kitu cha nyongeza kwa kocha lakini kitu muhimu ni kuweza kufundisha soka. Kutokana na dhana hiyo tumeweza kuwaona makocha wengi vijana wakifanya vyema katika vilabu tofauti duniani. Kuonekana kwao kunafanya kuondoa ile dhana ya awali kuwa ili uwe kocha mzuri lazima upitie katika kusakata soka katika madaraja ya juu.
Mohammed Kijuso
Katika klabu ya Mbeya City kwa muda mrefu Mara tu ya kuondoka kocha msaidizi Maka Mwalwisi waliamua kumpa jukumu lile aliyekuwa mchezaji wao Mohammed Kijuso.Akiwa kama kocha msaaidizi alifanya kazi na Juma Mwambusi kama kocha mkuu na baadae Kufanya kazi na Kinnah Phiri. Kwasasa baada ya klabu kuachana na kinnah Phiri majukumu yanakabidhiwa kwa Kijuso.
Akiwa na umri wa miaka 38, usije ukashangaa matokeo bora uwanjani yakawafanya halmashauri ya jiji la Mbeya kuamua kumpa jukumu la kocha wa klabu.Japo Kijuso amecheza soka katika daraja la juu kabisa kwa Tanzania lakini umri wake unamfanya aonekane kocha kijana na kubeba majukumu katika klabu yenye mashabiki wenye ushawishi mkubwa katika klabu yao.
Hivyo makala MAKOCHA VIJANA, WANAVYOFUNGUA AKILI ZA WAPENZI WA SOKA DUNIANI.
yaani makala yote MAKOCHA VIJANA, WANAVYOFUNGUA AKILI ZA WAPENZI WA SOKA DUNIANI. Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala MAKOCHA VIJANA, WANAVYOFUNGUA AKILI ZA WAPENZI WA SOKA DUNIANI. mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/09/makocha-vijana-wanavyofungua-akili-za.html
0 Response to "MAKOCHA VIJANA, WANAVYOFUNGUA AKILI ZA WAPENZI WA SOKA DUNIANI."
Post a Comment