title : Tanzania ya Kwanza Kutumia Mfumo wa PlanRep Kusini mwa Afrika
kiungo : Tanzania ya Kwanza Kutumia Mfumo wa PlanRep Kusini mwa Afrika
Tanzania ya Kwanza Kutumia Mfumo wa PlanRep Kusini mwa Afrika
Tanzania imetajwa kuwa nchi ya kwanza Kusini mwa Afrika kuanza kutumia mfumo wa kielektroniki wa PlanRep ulioboreshwa ambao husaidia katika mipango, bajeti na kutoa taarifa ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo nchini kote.
Akizungumza katika mahojiano maalum mjini Kigoma, Mkuu wa Timu ya Mifumo ya TEHAMA kutoka mradi wa Uimarishaji Mifumo ya Sekta za Umma (PS3) Desderi Wengaa, amesema kuwa mfumo huo utasaidia Taifa kufikia maendeleo endelevu kwa wakati kwani utaunganishwa na mifumo mingine iliyopo sasa na utawashirikisha wananchi wote.
“Mfumo huu utawezesha kutolewa kwa taarifa za miradi ya maendeleo zinazohusu sekta zote zilizoainishwa katika mipango na bajeti kwa wakati katika kipindi chote cha mwaka” alisema Wengaa.
Aliendelea kusema kuwa PlanRep iliyoboreshwa inaunganisha sekta zote katika mfumo mmoja ambao ni wa kitaifa tofauti na ilivyokuwa awali ambapo kila sekta ilikuwa na mfumo wake. Awali mfumo uliokuwa ukitumika haukuwa unaendana na mahitaji ya wakati hivyo kushindwa kufanya uchambuzi wa kina katika kusimamia rasilimali zilizokuwepo ikiwemo fedha.
Aidha,watumiaji wa mfumo huo wataweza kuutumia mahali popote kwa kuwa ni wa kitaifa na utaondoa changamoto ya kuwepo kwa matoleo tofauti tofauti. Hali hii itasaidia kuokoa fedha nyingi zilizokuwa zikitumika kwa watoa huduma wa mifumo ya awali katika halmashauri na mikoa yote nchini.
Kiongozi wa Timu ya wataalamu wanaofanya maboresho ya mfumo wa kielektroniki wa PlanRep, Bi. Nseya Kipilyango akizungumza wakati wa mafunzo kwa watumiaji wa mfumo huo yanayoendelea Mjini Kigoma.
Mmoja wa Wawezeshaji wa Mfumo wa mfumo wa kielektroniki wa PlanRep Kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Bi Jacqueline Manyanga akiwasilisha mada kwa watumiaji wa mfumo huo yanayofanyika Mkoani Kigoma yakihusisha Mikoa ya Rukwa, Katavi na Kigoma.
Washiriki wa Mafunzo wakifuatilia mada wakati wa mafunzo hayo yanayoendelea mjini Kigoma.
Hivyo makala Tanzania ya Kwanza Kutumia Mfumo wa PlanRep Kusini mwa Afrika
yaani makala yote Tanzania ya Kwanza Kutumia Mfumo wa PlanRep Kusini mwa Afrika Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala Tanzania ya Kwanza Kutumia Mfumo wa PlanRep Kusini mwa Afrika mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/08/tanzania-ya-kwanza-kutumia-mfumo-wa.html
0 Response to "Tanzania ya Kwanza Kutumia Mfumo wa PlanRep Kusini mwa Afrika"
Post a Comment