title : TUMEPUNGUZA UHALIFU KWA ASILIMIA 24.4 - RPC ARUSHA
kiungo : TUMEPUNGUZA UHALIFU KWA ASILIMIA 24.4 - RPC ARUSHA
TUMEPUNGUZA UHALIFU KWA ASILIMIA 24.4 - RPC ARUSHA
Na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi, Arusha
Jeshi la Polisi mkoani hapa limefanikiwa kupunguza makosa ya jinai kwa mwaka huu 2017 toka 1,378 yaliyoripotiwa mwaka jana 2016 hadi kufikia 1,041 na kufanya idadi ya makosa yaliyopungua kufikia 337.
Akitoa takwimu hizo ofisini kwake jana mchana, Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Naibu Kamishna (DCP) Charles Mkumbo (pichani), alisema kwamba punguzo hilo ni sawa na asilimia 24.4 huku akifafanua kwamba takwimu hizo ni kwa mujibu wa kuanzia mwezi Januari hadi Juni mwaka huu 2017.
“Huu upungufu wa makosa ya jinai ni takwimu za nusu mwaka, toka Januari hadi Juni mwaka huu 2017 ikilinganishwa na mwaka 2016 kwa muda kama huo, hivyo utaona tumejitahidi “. Alifafanua Kamanda Mkumbo, huku akiendelea kubainisha.
“Mwaka jana kwa nusu mwaka makosa ya mauaji yalikuwa 45 lakini mwaka huu kwa kipindi kama hicho makosa yalikuwa 36 pungufu ya makosa 9, wakati makosa ya kubaka yalikuwa 106 kwa mwaka jana lakini mwaka huu yameshuka hadi kufikia makosa 79 pungufu ya makosa 27, huku makosa ya unyang’anyi wa kutumia silaha mwaka jana yalikuwa makosa 16 na mwaka huu kwa kipindi kama hicho yamekuwa makosa matatu sawa na upungufu wa makosa 13”. Alisema Kamanda Mkumbo.
Hivyo makala TUMEPUNGUZA UHALIFU KWA ASILIMIA 24.4 - RPC ARUSHA
yaani makala yote TUMEPUNGUZA UHALIFU KWA ASILIMIA 24.4 - RPC ARUSHA Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala TUMEPUNGUZA UHALIFU KWA ASILIMIA 24.4 - RPC ARUSHA mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/07/tumepunguza-uhalifu-kwa-asilimia-244.html
0 Response to "TUMEPUNGUZA UHALIFU KWA ASILIMIA 24.4 - RPC ARUSHA"
Post a Comment