WADAU WA PSPF WAWATANGAZIA FURSA WASTAAFU WATARAJIWA

WADAU WA PSPF WAWATANGAZIA FURSA WASTAAFU WATARAJIWA - Hallo rafiki WORLD MAELEZO LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa WADAU WA PSPF WAWATANGAZIA FURSA WASTAAFU WATARAJIWA, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala biashara, makala general, makala hobby, makala karibuni info, makala michezo, makala siasa, makala utamaduni, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : WADAU WA PSPF WAWATANGAZIA FURSA WASTAAFU WATARAJIWA
kiungo : WADAU WA PSPF WAWATANGAZIA FURSA WASTAAFU WATARAJIWA

soma pia


WADAU WA PSPF WAWATANGAZIA FURSA WASTAAFU WATARAJIWA

NA K-VIS BLOG/Khalfan Said, Mwanza
MFUKO wa Pensheni wa PSPF umewaleta poamoja watumishi wa umma kutoka wilaya zote za mkoa wa Mwanza zaidi ya 450, ambao wanatarajiwa kustaafu hivi karibuni ili kuwapatia semina ya mafunzo itakayowawezwesha kujiandaa kustaafu kwa amani.
Katika semina hiyo iliyoanza leo Juni 2, 2017 kwenye ukumbi wa chuo cha BoT Capri-point  jijini Mwanza, wadau wa PSPF ambao ni taasisi za fedha nao wametumia fursa hiyo kutangaza fursa mbalimbali ambazo wastaafu hao wanaweza kuzitumia ili kuendeleza maisha yao ya baadaye.
Wadau hao ni pamoja na Mwalimu Commercial Bank, (MCB), NMB, CRDB, TPB na Mfuko wa UTT-AMIS, pia Shirika la Viwanda Vidogovidogo SIDO.
Mkuu wa Kitengo cha Biashara na Masoko, Mwalimu Commercial Bank, (MCB),Bw. Valence Luteganya, akizungumzia huduma mbalimbali zitolewazo na benki hiyo. "Beni hii imeanzishwa hivi karibuni na wamiliki wa benki hii kwa karibu asilimia 30 ni walimu. na huduma tunazozitoa ni pamoja na utoaji mikopo nafuu, ushauri wa kifedha lakini pia katika jiyihada za kurahisisha huduma za kibenki, MCB imo kwenye mtandao wa Umoja Switch ambao umetapakaa nchi nzima." hayo ni baadhi ya maneno ya Bw. Lutenganya
 Bw. Lutenganya, akifafanua zaidi huduma zitolewazo na benki ya MCB

Mkuu wa kitengo cha  wateja binafsi benki ya NMB, Bw.Omary Mtiga, akitoa somo kuhusu fursa mbalimbali ambazo wastaafu hao watarajiwa wanaweza kuzipata. "Benki ya NMB ina matawi kote nchini na hivyo inaweza kukufikishia huduma hapo ulipo pasina shaka, kwenu nyinyi ambao wengi wenu ni wateja wetu, mnayo fursa ya kufungua Bonas account ambayo inakuwezesha kufikia malengo mbalimbali uliyojiwekea na inaweza kutunza amana zako kwa usalama na kufikia malengo yako ya baadaye uliyojiwekea, lakini kubwa zaidi hakuna gharama za kuendesha akaunti hii." alisema
 Mkurugenzi wa idara ya mikopo benki ya Posta Tanzania, (TPB), Bw. Henry Bwogi, akizoa mada kwa washiriki ambapo alisema, "TPB ndiyo benki kongwe kuliko zote hapa nchini ikiwa na matawi yaliyosambaa kila kona ya nchi na hivyo kuwa rahisi kwa wateja kufikiwa na huduma zake, lakini pia benki hiyo tayari imeonyesha nia ya dhati ya kuwajali wastaaafu ambapo imekwisha toa mikopo ya mabilioni ya shilingi kwa wanachama wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF.
 Bi Doris Mlenge, Afisa Masoko wa Mfuko wa UTT-AMIS, akiwapatia vipeperushi vyenye maelezo ya huduma mbalimbali zitolewazo na Mfuko huo. "Kwa mtu yeyote anayetegemea kupata kipato kwa mkupuo kutokana na pensheni au chanzo kingine cha fedha anatakiwa kuwekeza kwenye Mfuko huo ili aweze kupata kipato cha mara kwa mara na akasema kuwekeza kwenye mifuko ya kujikimu kama UTT-AMIS kunatoa faida kubwa ukilinganisha na uwekezaji wa namna hiyo kwenye masoko ya fedha.


Hivyo makala WADAU WA PSPF WAWATANGAZIA FURSA WASTAAFU WATARAJIWA

yaani makala yote WADAU WA PSPF WAWATANGAZIA FURSA WASTAAFU WATARAJIWA Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala WADAU WA PSPF WAWATANGAZIA FURSA WASTAAFU WATARAJIWA mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/06/wadau-wa-pspf-wawatangazia-fursa.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "WADAU WA PSPF WAWATANGAZIA FURSA WASTAAFU WATARAJIWA"

Post a Comment