Rais wa zamani wa Botswana Ketumile Masire afariki dunia

Rais wa zamani wa Botswana Ketumile Masire afariki dunia - Hallo rafiki WORLD MAELEZO LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Rais wa zamani wa Botswana Ketumile Masire afariki dunia, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala biashara, makala general, makala hobby, makala karibuni info, makala michezo, makala siasa, makala utamaduni, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Rais wa zamani wa Botswana Ketumile Masire afariki dunia
kiungo : Rais wa zamani wa Botswana Ketumile Masire afariki dunia

soma pia


Rais wa zamani wa Botswana Ketumile Masire afariki dunia

Botswana imetangaza siku tatu za maombolezi ya kitaifa kufuatia kifo cha rais wa zamani wa nchi hiyo, Sir Ketumile Masire,  akiwa na miaka 91.
Sir Ketumile, aliongoza taifa hilo kuanzia 1980 hadi 1998, na amekuwa akisifiwa kwa kuchangia pakubwa katika kuweka msingi imara wa uthabiti wa kisiasa katika taifa hilo, shirika la AFP linasema.Alishiriki pia katika mikakati ya kufanikisha amani katika mataifa kadha Afrika, ikiwa ni pamoja na kufikisha kikomo vita vya wenyewe kwa wenyewe vya muda mrefu nchini Msumbiji.
Botswana ni moja ya nchi tajiri na thabiti zaidi barani Afrika.Sir Ketumile alichukua uongozi kufuatia kifo cha rais wa kwanza wa Botswana baada ya uhuru Sir Seretse Khama mwaka 1980.Alitumikia taifa hilo kama waziri wake wa kwanza wa fedha na baadaye kama makamu wa rais kabla ya kuwa rais.
Sir Ketumile alistaafu 1998 baada ya kuongoza taifa hilo katika kipindi cha ukuaji mkubwa wa kiuchumi na usimamizi mwema wa utajiri wa almasi wa Botswana.Aidha, alishiriki katika kuunga mkono vita dhidi ya serikali ya ubaguzi wa rangi Afrika Kusini na kuunga mkono pia harakati za kupigania uhuru katika mataifa mengine ya kanda hiyo.
Kama kiongozi mstaafu, alishiriki katika juhudi za upatanisho kote Afrika, ikiwa ni pamoja na nchini Kenya, Lesotho, Swaziland na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.Sir Ketumile alikuwa pia mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Watu Wastahiki ambalo lilichunguza mauaji ya kimbari ya Rwanda ya mwaka 1994. CHANZO BBC



Hivyo makala Rais wa zamani wa Botswana Ketumile Masire afariki dunia

yaani makala yote Rais wa zamani wa Botswana Ketumile Masire afariki dunia Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Rais wa zamani wa Botswana Ketumile Masire afariki dunia mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/06/rais-wa-zamani-wa-botswana-ketumile.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "Rais wa zamani wa Botswana Ketumile Masire afariki dunia"

Post a Comment