NSSF YAKABIDHI HUNDI YA SHILINGI BILIONI 1.5 UPANUZI WA KIWANDA CHA CHAKI SIMIYU

NSSF YAKABIDHI HUNDI YA SHILINGI BILIONI 1.5 UPANUZI WA KIWANDA CHA CHAKI SIMIYU - Hallo rafiki WORLD MAELEZO LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa NSSF YAKABIDHI HUNDI YA SHILINGI BILIONI 1.5 UPANUZI WA KIWANDA CHA CHAKI SIMIYU, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala biashara, makala general, makala hobby, makala karibuni info, makala michezo, makala siasa, makala utamaduni, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : NSSF YAKABIDHI HUNDI YA SHILINGI BILIONI 1.5 UPANUZI WA KIWANDA CHA CHAKI SIMIYU
kiungo : NSSF YAKABIDHI HUNDI YA SHILINGI BILIONI 1.5 UPANUZI WA KIWANDA CHA CHAKI SIMIYU

soma pia


NSSF YAKABIDHI HUNDI YA SHILINGI BILIONI 1.5 UPANUZI WA KIWANDA CHA CHAKI SIMIYU

Waziri wa Nchi Ofisi Waziri Mkuu Sera, Bunge,Kazi, Ajira,Vijana na wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama(kulia) akimkabidhi hundi ya shilingi bilioni 1.5 zilizotolewa na NSSF kama mkopo kwa ajili ya upanuzi wa kiwanda cha chaki Maswa, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa, Dkt.Fredrick Sagamiko.

Na Stella Kalinga, Simiyu

Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) umekabidhi hundi ya shilingi bilioni 1.5 kwa Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Mkoani Simiyu, fedha ambazo ni mkopo kwa ajili ya upanuzi wa kiwanda cha Chaki Wilayani humo na kuongeza uzalishaji.

Hundi hiyo imekabidhiwa kwa Waziri wa Nchi Ofisi Waziri Mkuu Sera, Bunge,Kazi, Ajira,Vijana na wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama kwa niaba ya Serikali na Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Prof.Godius Kahyarara wilayani Maswa mkoani Simiyu.


Akizungumza wakati wa makabidhiano ya hundi hiyo Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Prof.Godius Kahyarara amepongeza Mkoa wa Simiyu kwa kutekeleza Sera ya Ujenzi wa Uchumi wa Viwanda kwa vitendo na kuwataka viongozi wa mkoa huo kutokatishwa tamaa.

Amesema NSSF kama Shirika la Umma linatekeleza sera na maelekezo ya Serikali na wametoa mkopo huo kwa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa ili wafanye upanuzi wa kiwanda cha chaki na kuongeza uzalshaji kwa kuwa suala la Viwanda ni la kipaumbele.
Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Prof.Godius Kahyarara(kushoto) akimkabidhi Waziri wa Nchi Ofisi Waziri Mkuu Sera, Bunge,Kazi, Ajira,Vijana na wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama hundi ya shilingi bilioni 1.5 zilizotolewa na NSSF kama mkopo kwa ajili ya upanuzi wa kiwanda cha chaki Maswa, (kulia) Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka.

Waziri wa Nchi Ofisi Waziri Mkuu Sera, Bunge,Kazi, Ajira,Vijana na watu wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama amesema kiwanda cha Chaki Maswa kimebeba ujumbe na dhana ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli ya kushikamanisha Uchumi wa Viwanda na Maendeleo ya watu kwa sababu kinatumia malighafi ya hapa nchini.

Aidha, amesema kiwanda hiki kitawanufaisha Watanzania hususani vijana wa Mkoa wa Simiyu ambao watafanya kazi moja moja katika kiwanda na wale wataohusika katika uchimbaji wa malighafi ambayo inapatikana maeneo mengine hapa nchini.
Waziri wa Nchi Ofisi Waziri Mkuu Sera, Bunge,Kazi, Ajira,Vijana na wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama akipokea taarifa ya Upembuzi yakinifu wa panuzi wa kiwanda cha chaki cha Maswa kutoka kwa mtalaam wa Taasisi ya Masuala ya Kiuchumi na Kijamii(ESRF), Deodatus Sagamiko.

“Asilimia 56 ya nguvukazi hapa Tanzania ni vijana na vijana wengi bado hawana ajira lakini kiwanda hiki kitasaidia, kwa kuwa sehemu ya hiyo asilimia 56 wataajiriwa katika kiwanda na wengine watapata ajira huko mkoani Singida ambako malighafi ya kutengenezea chaki inapatikana” amesema.



Hivyo makala NSSF YAKABIDHI HUNDI YA SHILINGI BILIONI 1.5 UPANUZI WA KIWANDA CHA CHAKI SIMIYU

yaani makala yote NSSF YAKABIDHI HUNDI YA SHILINGI BILIONI 1.5 UPANUZI WA KIWANDA CHA CHAKI SIMIYU Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala NSSF YAKABIDHI HUNDI YA SHILINGI BILIONI 1.5 UPANUZI WA KIWANDA CHA CHAKI SIMIYU mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/06/nssf-yakabidhi-hundi-ya-shilingi.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "NSSF YAKABIDHI HUNDI YA SHILINGI BILIONI 1.5 UPANUZI WA KIWANDA CHA CHAKI SIMIYU"

Post a Comment