title : MFUMO WA USAJILI NCHINI KUBORESHWA
kiungo : MFUMO WA USAJILI NCHINI KUBORESHWA
MFUMO WA USAJILI NCHINI KUBORESHWA
Serikali ya Tanzania inafanya maboresho ya Mfumo wa Usajili uliopo na kuanzisha mfumo utakaofanya kazi vizuri usajili wa matukio muhimu ya binadamu na takwimu nchini unaofanywa na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini - RITA
Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi amesema hayo mjini Dodoma wakati akifungua mkutano wa wadau wanaojadili mfumo huo. Amesema maboresho ya mfumo huo yanatekelezwa kupitia Mkakati wa Kitaifa wa usajili wa Matukio muhimu ya binadamu na takwimu (Civil Registration and Vital STATISTICS-CVRS.
Prof Kabudi amesema Mfumo huo unalenga kutatua changamoto mbalimbali ambazo zimefanya hali ya usajili wa Matukio muhimu ya binadamu kutokuwa ya kuridhisha nchini. Ameongeza kuwa ana imani kuwa utekelezaji wa mkakati huo itakuwa njia sahihi itakayowezesha kumuona kila mwananchi katika picha ya taifa.
Mkutano huo wa wadau wa usajili wa Matukio muhimu ya mwanadamu nchini umeandaliwa na RITA
Waziri Prof. Kabudi akipata picha na washiriki baada ya kufungua mkutano wa wadau wanaojadili mfumo huo. Amesema maboresho ya mfumo huo yanatekelezwa kupitia Mkakati wa Kitaifa wa usajili wa Matukio muhimu ya binadamu na takwimu (Civil Registration and Vital STATISTICS-CVRS.
Hivyo makala MFUMO WA USAJILI NCHINI KUBORESHWA
yaani makala yote MFUMO WA USAJILI NCHINI KUBORESHWA Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala MFUMO WA USAJILI NCHINI KUBORESHWA mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/06/mfumo-wa-usajili-nchini-kuboreshwa.html
0 Response to "MFUMO WA USAJILI NCHINI KUBORESHWA"
Post a Comment