title : MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA SPORTPESA
kiungo : MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA SPORTPESA
MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA SPORTPESA
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan amekubali ombi la kuwa mgeni rasmi katika mchezo kirafiki kati ya Timu ya Everton ya nchini Uingereza na timu ya Gor Mahia ya Kenya ambayo ilitwaa kombe la michuano ya Sportpesa iliyofayika hapa nchini hivi karibuni.
Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amekubali ombi hilo baada ya Kukutana na kufanya mazungumzo na Watendaji wa Kampuni inayojishughulisha na ubashiri wa michezo ya Sports Betting nchini ambao waliongozwa na Mkurugenzi wa Utawala na Utekelezaji Tarimba Abbas Ikulu- Dar es Salaam.
Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amepongeza mipango na mikakati mizuri ya kampuni hiyo ya kutaka kukuza vipaji vya wanamichezo hasa kwa mpira wa miguu kwa Tanzania Bara na Zanzibar na kusema kama malengo hayo yatafikiwa Tanzania itakuwa bora katika mchezo wa mpira wa katika bara la Afrika na Dunia kwa ujumla.
Makamu wa Rais pia amewahakikishia watendaji wa kampuni hiyo kuwa milango ya ofisi yake ipo wazi na pindi wakiwama katika jambo lolote wawasiliane na ofisi yake ili tatizo linalowakabili liweze kutafutiwa ufumbuzi ili lisikwamishe shughuli za kampuni hiyo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya ubashiri wa michezo ya SportPesa Bw. Pavel Slavkov (kushoto), katikati ni Mkurugenzi wa Utawala na Utekelezaji Bw. Abbas Tarimba.Viongozi hao wa SportPesa walimtembelea Makamu wa Rais Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Viongozi wa SportPesa waliofika ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo kwa lengo la kujitambulisha.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi wa SportPesa Tanzania.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Hivyo makala MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA SPORTPESA
yaani makala yote MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA SPORTPESA Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA SPORTPESA mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/06/makamu-wa-rais-akutana-na-sportpesa.html
0 Response to "MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA SPORTPESA"
Post a Comment