title : UWT UNGUJA WATAKIWA KUPAMBANA KWA NGUVU ZOTE KULINDA MASLAHI YA CCM.
kiungo : UWT UNGUJA WATAKIWA KUPAMBANA KWA NGUVU ZOTE KULINDA MASLAHI YA CCM.
UWT UNGUJA WATAKIWA KUPAMBANA KWA NGUVU ZOTE KULINDA MASLAHI YA CCM.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Samia Suluhu Hassan akizungumza na wajumbe wa Kamati tekelezaji za UWT ngazi za Wilaya, Mikoa na Taifa Unguja, huko Afisi Kuu Kisiwandui.
…………
NA MWANDISHI WETU, ZANZIBAR.
JUMUIYA ya Wanawake wa CCM (UWT) wametakiwa kutumia uwezo, weledi, nguvu na ushawishi waliokuwa nao kisiasa kuhakikisha Chama cha Mapinduzi kinafanikisha kwa ufanisi Uchaguzi wa ndani ya Chama ili ipatikane timu imara ya viongozi watakaofanikisha Ushindi wa Dola katika Uchaguzi Mkuu 2020.
Nasaha hizo zimetolewa na Mjumbe wa Kamati Kuu wa CCM, Mh. Samia Suluhu Hassan wakati akizungumza na Wajumbe wa Kamati Tekelezaji wa ngazi za Wilaya, Mikoa hadi Taifa wa UWT, huko Afisi Kuu CCM Kisiwandui Zanzibar alipohitimisha ziara yake ya kuimarisha Chama hicho nchini.
Alifafanua kwamba UWT wanatakiwa kwa mstari wa mbele kuhakikisha kila hatua ya uchaguzi huo inafanyika kwa ufanisi kwa lengo la kupata jopo la viongozi na watendaji waadilifu na wenye uwezo wa kusoma alama za nyakati kisiasa na kijamii.
Pia aliendelea kueleza kwamba wanawake wa Umoja huo ni miongoni mwa rasilimali watu wanaotakiwa kukitumikia chama kwa bidii ili kiweze kufikia malengo yake ya kuendeleza ushindi wa Dola kwa kila uchaguzi mkuu wa kisiasa.
Mh. Ambaye pia ni Makamo wa Pili wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, aliwambia Akina Mama hao kwamba mikakati hiyo itafanyika kwa ufanisi endapo kila mtu ndani ya umoja huo atakuwa tayari kutumia kipaji chake cha kisiasa kuhakikisha analinda na kutetea maslahi ya chama kwa vitendo.
“ Wanawake tutumieni uwezo wetu katika kujenga ushawishi na hamasa kwa kuongeza wanachama wapya watakaokubali kuwa na itikadi ya kweli ya CCM.
Pamoja na mipango yetu ya kuimarisha chama tusisahau kuzidisha umoja na upendo miongoni mwetu kwa kuacha baadhi ya mambo yasiyofaa na tunayohisi hayana maslahi na Chama pamoja na jumuiya yetu”, alisema Mh.Samia na kuongeza kuwa lazima viongozi waliopewa dhamana ndani ya umoja huo wafanye kazi kwa bidii ili wananchi waendelee kujivunia uwepo wa Chama hicho katika medali za kisisasa Visiwani Zanzibar.
Pamoja na hayo alisisitiza umuhimu wa wanachama wa chama hicho hasa Wazee kuwarithisha watoto wao miongozo na itikadi za ASP ambayo ni CCM, ili waweze kukua wakiwa katika misingi ya weledi na ukada wa kweli ambazo ni nyenzo zitakazowasaidia pindi watakapokuwa viongozi wa chama na serikali wa baadae.
Hata hivyo aliwataka viongozi na watendaji kuhakikisha takwimu za wanachama wanazoratibu zinakuwa sahihi ili ziweze kusaidia katika tathimini mbali mbali za kisiasa nchini hasa kabla na baada ya uchaguzi.
Akitoa ufafanuzi juu ya Uchaguzi wa chama unaoendelea kwa hatua ya uchukuaji wa fomu kwa ngazi ya Matawi na mashina, Katibu wa NEC, Idara ya Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar, Bi. Waride Bakar Jabu amesema nafasi zinazochukuliwa fomu kwa mtu mmoja ni zile za kiutendaji ambazo ni Katibu na Mwenyekiti lakini nafasi zingine zote zilizobaki zinatakiwa kuchukuliwa fomu zaidi ya mtu mmoja.
Akizungumza katika kikao hicho, Kaimu Naibu Katibu Mkuu wa UWT Zanzibar , Bi. Tunu Juma Kondo alisema umoja huo umekuwa ukishiriki ipasavyo katika majukumu mbali mbali ya chama na kuhakikisha yanafanyikana na kukamilika kwa wakati.
Aidha aliahidi kwamba umoja huo utafanya kila linalowezekana kuhakikisha Uchaguzi ndani ya taasisi hiyo unafanyika vizuri kwa mujibu wa kanuni na miongozo ya Katiba ya CCM ya mwaka 1977 pamoja na marekebisho yake.
Naye Waziri wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto Bi. Maudline Cyrus Castico, akitoa ufafanuzi juu ya kesi za udhalilishaji wa kijinzia nchini, alisema kwa sasa wanaendelea na kutoa elimu kwa jamii juu ya kuwa na muamuko wa kutoa ushahidi mahakamani huku wakiandaa mikakati imara ya kusimamia vyombo vya kisheria vitende haki kwa watu wanaofanya uhalifu huo.
Kwa upande wao viongozi mbali mbali wa umoja huo kutoka Mikoa ya Zanzibar kichama walipewa fursa ya kutoa maoni na ushauri wao, ambao walipendekeza kwamba CCM kupitia idara husika ziendeleze madarasa ya Itikadi kwa vijana mbali mbali ili kupata viongozi wa baadae walioiva kisiasa.
Akizungumza miongoni mwa waasisi wa ASP, Bi.Asha Simba aliwataka vijana wa Chama hicho kuvaa joho la Vijana wa enzi za ASP waliokomboa Zanzibar kutoka katika mikono ya utawala wa kimabavu, na wao wafuate nyayo hizo kuendeleza heshima ya CCM kwa sasa.
Hivyo makala UWT UNGUJA WATAKIWA KUPAMBANA KWA NGUVU ZOTE KULINDA MASLAHI YA CCM.
yaani makala yote UWT UNGUJA WATAKIWA KUPAMBANA KWA NGUVU ZOTE KULINDA MASLAHI YA CCM. Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala UWT UNGUJA WATAKIWA KUPAMBANA KWA NGUVU ZOTE KULINDA MASLAHI YA CCM. mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/04/uwt-unguja-watakiwa-kupambana-kwa-nguvu.html
0 Response to "UWT UNGUJA WATAKIWA KUPAMBANA KWA NGUVU ZOTE KULINDA MASLAHI YA CCM."
Post a Comment