title : Dkt. Susan Kolimba akutana na Balozi wa Uingereza nchini
kiungo : Dkt. Susan Kolimba akutana na Balozi wa Uingereza nchini
Dkt. Susan Kolimba akutana na Balozi wa Uingereza nchini
Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Susan Kolimba akizungumza na Balozi wa Uingereza nchini, Mhe. Sarah Cooke alipomtembelea leo katika ofisi za Wizara. Katika mzungumzo yao Mhe. Kolimba alieleza nia ya Serikali ya Tanzania katika kuimarisha ushirikiano na Serikali ya Uingereza sambamba na kuzungumzia miradi mbalimbali inayotekelezwa na serikali yake katika kuwaletea maendeleo na kuboresha maisha ya watanzania.
Mhe. Sarah akimweleza Mhe. Kolimba malengo ya Serikali ya Uingereza katika kuimarisha maeneo ya ushirikiano hususan katika sekta ya kilimo, elimu, afya sambamba na ujenzi wa miundombinu.
Mazungumzo yakiendelea, kulia ni maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje wakifuatilia mazungumzo hayo.
Hivyo makala Dkt. Susan Kolimba akutana na Balozi wa Uingereza nchini
yaani makala yote Dkt. Susan Kolimba akutana na Balozi wa Uingereza nchini Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala Dkt. Susan Kolimba akutana na Balozi wa Uingereza nchini mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/04/dkt-susan-kolimba-akutana-na-balozi-wa.html
0 Response to "Dkt. Susan Kolimba akutana na Balozi wa Uingereza nchini"
Post a Comment