title : DKT. NCHIMBI AZITAKA KAMATI ZA MAJI KUSIMAMIA KIMAMILIFU MIRADI YA MAJI MANISPAA YA SINGIDA.
kiungo : DKT. NCHIMBI AZITAKA KAMATI ZA MAJI KUSIMAMIA KIMAMILIFU MIRADI YA MAJI MANISPAA YA SINGIDA.
DKT. NCHIMBI AZITAKA KAMATI ZA MAJI KUSIMAMIA KIMAMILIFU MIRADI YA MAJI MANISPAA YA SINGIDA.
Kamati za maji za visima kumi vya maji katika manispaa ya Singida zimekuwa sababu ya miradi hiyo iliyokamilika kwa asilimia miamoja kutofanya kazi na kuwanufausha wananchi huku ikiwa imegharimu fedha nyingi za serikali na wahisani hasa benki ya dunia.
Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi mwishoni mwa wiki hii mara baada ya kukagua miradi hiyo na kujiridhisha kuwa miradi hiyo imekamilika licha ya kutofanya kazi.
Dkt. Nchimbi amesema sababu kubwa ya kutofanya kazi miradi hiyo ni udhaifu wa kamati za maji na wanasiasa katika maeneo ya miradi kutojali shida ya wananchi ya kukosa maji na hivyo kuitelekeza miradi hiyo badala ya kuisimamia.
Amesema lengo la miradi hiyo ni wananchi wapate maji safi na salama kwa umbali usiozidi kilometa nne kama ilivyoagizwa na serikali.
“Katika ukaguzi wangu nimebaini mifumo katika miradi hii ya maji ipo vizuri sana. Baadhi inaendeshwa kwa umeme na mingine kwa mafuta ya dizel. Makubaliano yalikuwa baada ya kukamilika miradi hii iendeshwe na kamati za maji kwa asilimia mia moja”, amesema.
Dkt. Nchimbi amesema wajibu wa kamati hizo ni pamoja na kukusanya fedha zinazotokana na kuuza maji kwa wateja pamoja na matengenezo ya miundombinu ya visima hivyo ili miradi hiyo iwe endelevu.
“Fedha zinazopatikana ndizo zitakazoendesha mradi husika ikiwemo kugharamia matengenezo ya mashine, pampu, miundombinu, kununulia dizel, umeme na kumlipa mhudumu wa mradi. Makubaliano ni miradi ikikamilika inabaki mikononi mwa wananchi kupitia kamati zao za maji. Serikali na wafadhili hawatahusika tena”, amesisitiza Dkt. Nchimbi.
Hivyo makala DKT. NCHIMBI AZITAKA KAMATI ZA MAJI KUSIMAMIA KIMAMILIFU MIRADI YA MAJI MANISPAA YA SINGIDA.
yaani makala yote DKT. NCHIMBI AZITAKA KAMATI ZA MAJI KUSIMAMIA KIMAMILIFU MIRADI YA MAJI MANISPAA YA SINGIDA. Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala DKT. NCHIMBI AZITAKA KAMATI ZA MAJI KUSIMAMIA KIMAMILIFU MIRADI YA MAJI MANISPAA YA SINGIDA. mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/04/dkt-nchimbi-azitaka-kamati-za-maji_30.html
0 Response to "DKT. NCHIMBI AZITAKA KAMATI ZA MAJI KUSIMAMIA KIMAMILIFU MIRADI YA MAJI MANISPAA YA SINGIDA."
Post a Comment