Dkt. Mwakyembe: BMT waiteni TASWA kujadili Katiba kabla ya Uchaguzi Mkuu

Dkt. Mwakyembe: BMT waiteni TASWA kujadili Katiba kabla ya Uchaguzi Mkuu - Hallo rafiki WORLD MAELEZO LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Dkt. Mwakyembe: BMT waiteni TASWA kujadili Katiba kabla ya Uchaguzi Mkuu, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala biashara, makala general, makala hobby, makala karibuni info, makala michezo, makala siasa, makala utamaduni, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Dkt. Mwakyembe: BMT waiteni TASWA kujadili Katiba kabla ya Uchaguzi Mkuu
kiungo : Dkt. Mwakyembe: BMT waiteni TASWA kujadili Katiba kabla ya Uchaguzi Mkuu

soma pia


Dkt. Mwakyembe: BMT waiteni TASWA kujadili Katiba kabla ya Uchaguzi Mkuu

Na Lorietha Laurence –WHUSM,Dar es Salaam.
Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe  amewataka watendaji wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) kuitisha kikao na viongozi wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo (TASWA)  pamoja na baadhi ya waandishi wa habari hizo kujadili na kupitia katiba ya chama hicho.
Dkt. Mwakyembe ametoa rai hiyo jana Jijini Dar es Salaam alipokutana na baadhi ya Waandishi wa Habari za michezo , alichokiitisha baada ya kupokea barua ya malalamiko  zinazoelezea changamoto mbalimbali zinazowakabili waandishi hao wa michezo.
“ Watendaji wa Baraza la Michezo la Taifa  waiteni viongozi wa TASWA wakiwemo na wawakilishi ambao ni waandishi wa habari za michezo  ili kupitia katiba inayokiongoza chama hicho kabla ya uchaguzi Mkuu” alisema Dkt. Mwakyembe.
Aliongeza kwa kueleza kuwa waandishi wa habari za michezo wana uhuru wa kuunda chama kipya endapo hawaridhishwi na utendaji wa TASWA ingawa kabla ya kufanya maamuzi yoyote, kikao kifanyike kwanza ili kufikia muafaka.
Alizidi kufafanua kuwa  waandishi wa habari za michezo ni muhimili muhimu katika sekta ya habari na maendeleao ya michezo  ndani na nje ya nchi, kwa kuwa mstari wa mbele katika kuhabarisha jamii  kuhusiana na masuala ya michezo.
Wakati huo huo, Dkt. Mwakyembe alipata nafasi ya kutembelea wasanii wa kikundi cha Nafasi Arts Space kilichopo Mikocheni B Jijini Dar es Salaam, ambapo alifurahishwa na kazi mbalimbali za sanaa zinazofanywa na kikundi hicho.
 Waziri wa Habari , Utamaduni, Sanaa na Michezo  Dkt. Harrison Mwakyembe (Kushoto) akifafanua jambo wakati wa mkutano na waandishi wa Habari za michezo kilichofanyika jana Uwanja wa Taifa  Jijini Dar es Salaam, kulia ni Afisa Habari wa TFF Cliford Ndimbo.
 Baadhi ya Waandishi wa Habari za michezo wakimsikiliza Waziri wa Habari , Utamaduni, Sanaa na Michezo  Dkt. Harrison Mwakyembe (Hayupo katika picha) katika kikao kilichofanyika jana Uwanja wa Taifa  Jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Habari , Utamaduni, Sanaa na Michezo  Dkt. Harrison Mwakyembe (Katikati) akipata maelekezo kutoka kwa Msanii wa Sanaa ya Uchoraji Bw. Ramadhani Mabera (kushoto) na kulia ni Mwalimu wa Sanaa za Uchoraji kutoka Zanzibar Bw. Abdulla Omar maarufu kama Dulla Wise.
 Waziri wa Habari , Utamaduni, Sanaa na Michezo  Dkt. Harrison Mwakyembe (Kushoto) akipokea zawadi ya picha ya kuchora kutoka kwa Mjumbe wa Bodi ya Nafasi Arts Space Bibi. Sauda Simba   baaada ya kuzungumza na wasanii hao jana Jijini Dar es Salaam.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA


Hivyo makala Dkt. Mwakyembe: BMT waiteni TASWA kujadili Katiba kabla ya Uchaguzi Mkuu

yaani makala yote Dkt. Mwakyembe: BMT waiteni TASWA kujadili Katiba kabla ya Uchaguzi Mkuu Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Dkt. Mwakyembe: BMT waiteni TASWA kujadili Katiba kabla ya Uchaguzi Mkuu mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/10/dkt-mwakyembe-bmt-waiteni-taswa.html

Subscribe to receive free email updates:

0 Response to "Dkt. Mwakyembe: BMT waiteni TASWA kujadili Katiba kabla ya Uchaguzi Mkuu"

Post a Comment