title : Vitabu Nilivyonunua Nairobi
kiungo : Vitabu Nilivyonunua Nairobi
Vitabu Nilivyonunua Nairobi
Nilisafiri tarehe 15 Julai mwaka huu kutoka Marekani kwenda Tanzania. Nilishukia Nairobi, kwa shughuli binafsi, ikiwemo kununua vitabu vya ki-Swahili. Kitabu nilichotamani zaidi ni Sauti ya Dhiki cha Abdilatif Abdalla ambacho nilitaka kukisoma kwa makini kuliko nilivyowahi kufanya kabla. Ninawazia pia kutafsiri kwa ki-Ingereza baadhi ya mashairi.
Nilivyoingia tu katika duka la vitabu la Textbbook Center, Kijabe Street, nilikitafuta kitabu cha Sauti ya Dhiki. Nilikiona, kikiwa na jalada tofauti na lile la mwaka 1973. Nilinunua pia Kichwamaji, Kaptula la Marx, na Dhifa, vya Euphrace Kezilahabi; Mashetani, tamthilia ya Ebrahim Hussein, na Haini, cha Adam Shafi. Tangu zamani, nimekuwa na baadhi ya vitabu vya Kezilahabi, Ebrahim Hussein, na Adam Shafi. Ninafurahi kujipatia vile ambavyo sikuwa navyo. Hata hivi, nimegundua kuwa sasa nina nakala mbili za Mashetani na mbili za Kichwamaji. |
Hivyo makala Vitabu Nilivyonunua Nairobi
yaani makala yote Vitabu Nilivyonunua Nairobi Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala Vitabu Nilivyonunua Nairobi mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/08/vitabu-nilivyonunua-nairobi.html
0 Response to "Vitabu Nilivyonunua Nairobi"
Post a Comment