title : Mfumo wa usimamizi wa fedha za umma(Epicor 10.2) kuboresha usimamizi wa mapato na matumizi kwenye Halmashauri nchini
kiungo : Mfumo wa usimamizi wa fedha za umma(Epicor 10.2) kuboresha usimamizi wa mapato na matumizi kwenye Halmashauri nchini
Mfumo wa usimamizi wa fedha za umma(Epicor 10.2) kuboresha usimamizi wa mapato na matumizi kwenye Halmashauri nchini
Daudi Manongi- MAELEZO, Iringa
Mfumo wa usimamizi wa fedha za umma (Epicor 10.2) utawajengea uwezo wahasibu na maafisa usimamizi wa fedha wa mikoa ili kusimamia vyema mapato na matumizi ya fedha za umma kwenye halmashauri zao.
Hayo yamesemwa leo Mkoani Iringa na Katibu tawala wa mkoa huo Bi Wamoja Ayubu wakati akifungua mafunzo ya mfumo huo Mkoani hapa.
"Mfumo wa Epicor 10.2 umeandaliwa mahsusi kuungana na mifumo mingine ili kukidhi matakwa ya maboresho yanayoendelea, Mafunzo haya yana lengo la kuwajengea uwezo ili muweze kusimamia fedha za umma na kuwapatia uelewa wa mabadiliko ya msingi yaliyofayika bila kukwamisha utoaji wa huduma kwa wananchi" Alisema Bi.Ayubu
Aidha ameeleza kuwa kupitia mafunzo haya wahasibu na maafisa usimamizi fedha wa mikoa wataelekezwa kwa ufupi namna mfumo wa epicor 10.2 utakavyobadilishana taarifa na mifumo ya mipango na bajeti (PlanRep) pamoja na mfumo wa FFARS na hivyo kuleta utejelezaji wa dhana nzima ya uwazi,uwajibikaji na utawala bora katika usmamizi wa fedha za umma.
Pamoja na hayo katibu tawala huyo ameishukuru TAMISEMI kwa kushirikiana na washirika wa maendeleo ambao ni mradi wa uimarishaji wa mifumo ya sekta za umma(PS3), kwa kazi nzuri inayofaywa na mradi huo kwa kuwezesha mafunzo hayo kufanyika mkoani Iringa.
Mkurugenzi Msaidizi Miundombinu ya TEHAMA-TAMISEMI Bw.Baltazar Kibola akifuatilia jambo wakati wa Mafunzo ya usimamizi wa fedha za umma kwa watumishi wa mikoa na mamlaka za Serikali za mitaa yaliyofanyika leo Mkoani Iringa.
Muhasibu kutoka Ofisi ya Rais-TAMISEMI Bi.Catherine Kiyuo akimwelekeza jambo mshiriki wa mafunzo ya usimamizi wa fedha za umma kwa watumishi kwa watumishi wa mikoa na mamlaka za Serikali za mitaa jinsi mfumo huo unavyofanya kazi leo Mkoani Iringa.
Washiriki wa Mafunzo ya Usimamizi wa fedha za Umma ambao wanajumuisha wahasibu na Maafisa usimamizi wa Fedha wa Mikoa mbalimbali wakifuatilia mafunzo hayo leo Mkoani Iringa.
Mhasibu kutoka Ofisi ya Rais-TAMISEMI Bw.Juma Shaha akielezea jinsi mfumo wa Usimamizi wa fedha za Umma ujulikanao kama Epicor 10.2 unavyofanya kazi kwa wahasibu na Maafisa usimamizi wa Fedha wa Mikoa mbalimbali leo Mkoani Iringa.
Mhasibu kutoka Mkoa wa Songwe Bw.David Johnson akielezea jinsi gani wahasibu na Maafisa usimamizi wa fedha wa mikoa wanavyoweza kusimamia mapato kwa kutumia mfumo wa Epicor 10.2 leo Mkoani Iringa.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Hivyo makala Mfumo wa usimamizi wa fedha za umma(Epicor 10.2) kuboresha usimamizi wa mapato na matumizi kwenye Halmashauri nchini
yaani makala yote Mfumo wa usimamizi wa fedha za umma(Epicor 10.2) kuboresha usimamizi wa mapato na matumizi kwenye Halmashauri nchini Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala Mfumo wa usimamizi wa fedha za umma(Epicor 10.2) kuboresha usimamizi wa mapato na matumizi kwenye Halmashauri nchini mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/06/mfumo-wa-usimamizi-wa-fedha-za.html
0 Response to "Mfumo wa usimamizi wa fedha za umma(Epicor 10.2) kuboresha usimamizi wa mapato na matumizi kwenye Halmashauri nchini"
Post a Comment