title : Ubalozi Kuwait wakabidhi kisima cha maji nambari 63 katika Chuo cha Ufundi cha Yombo kwa wanafunzi walemavu
kiungo : Ubalozi Kuwait wakabidhi kisima cha maji nambari 63 katika Chuo cha Ufundi cha Yombo kwa wanafunzi walemavu
Ubalozi Kuwait wakabidhi kisima cha maji nambari 63 katika Chuo cha Ufundi cha Yombo kwa wanafunzi walemavu
Balozi wa Kuwait nchini, Jasem Al-Najem hivi karibuni alizindua kisima cha maji safi na salama nambari 63 katika Chuo cha Ufundi cha Yombo kwa wanafunzi walemavu kilichopo Jijini Dar es salaam.
Uzinduzi huo ambao ulishuhudiwa na mwakilishi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Josephine Lyungi, Kaimu Mkuu wa Chuo, Bi. Maryam, Mwenyekiti wa Mtaa wa Kiwalani, Emannuel pamoja na walimu na wanafunzi.
Huu ni mwendelezo wa mradi ulioanzishwa na Ubalozi wa Kuwait unaofahamika kwa jina la “KISIMA CHA MAJI KATIKA KILA SHULE”. Katika hotuba fupi iliyotolewa na Balozi Najeem, alisema kuwa uzinduzi wa kisima hicho ni utekelezaji wa ahadi aliyoitoa mnamo tarehe Novemba 30, 2017 Chuoni hapo wakati wa uzinduzi wa "Mpango kamili wa kuwasaidia walemavu nchini Tanzania" wenye thamani ya dola laki tano kutoka Serikali ya Kuwait akiwa pamoja na Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu) Mhe. Jenista Mhagama ambaye alimuomba Balozi ajenge kisima kituoni hapo.
Kwa upande wake Mkuu wa Chuo, Bi. Maryam ameushukuru Ubalozi wa Kuwait kwa kuwajengea kisima ambacho kitawasaidia wanafunzi katika kufua, kuoga na kufanya usafi madarasani, mabwenini na maeneo mengine ya Chuo
Pembezoni mwa uzinduzi wa kisima cha maji, Al-Najem alitembea sehemu ya kujifunzia ushoni chuoni hapo kwa wanafunzi wenye ulemavu ambapo Ubalozi uliwahi kuchangia vyarahani katika ziara yake ya kwanza, na mara hii aliahidi kukipatia chuo hicho vitambaa na vifaa vyengine vinavyohitajika katika ushoni.
Balozi wa Kuwait nchini, Jasem Al-Najem akishuhudia wanafunzi wa Chuo cha Ufundi cha Yombo, wakiteka maji katika kisima alichokizindua hivi karibuni.
Sehemu ya Wanafunzi wa Chuo cha Ufundi cha Yombo wakiendela na mafunzo yao wakati, Balozi wa Kuwait nchini, Jasem Al-Najem alipowatembela.
Hivyo makala Ubalozi Kuwait wakabidhi kisima cha maji nambari 63 katika Chuo cha Ufundi cha Yombo kwa wanafunzi walemavu
yaani makala yote Ubalozi Kuwait wakabidhi kisima cha maji nambari 63 katika Chuo cha Ufundi cha Yombo kwa wanafunzi walemavu Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala Ubalozi Kuwait wakabidhi kisima cha maji nambari 63 katika Chuo cha Ufundi cha Yombo kwa wanafunzi walemavu mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/05/ubalozi-kuwait-wakabidhi-kisima-cha.html
0 Response to "Ubalozi Kuwait wakabidhi kisima cha maji nambari 63 katika Chuo cha Ufundi cha Yombo kwa wanafunzi walemavu"
Post a Comment