title : KATIBU MKUU PROF. ELISANTE OLE GABRIEL ATEMBELEA KIWANDA CHA HUANRI MEDICAL GROUP BEIJING NCHINI CHINA
kiungo : KATIBU MKUU PROF. ELISANTE OLE GABRIEL ATEMBELEA KIWANDA CHA HUANRI MEDICAL GROUP BEIJING NCHINI CHINA
KATIBU MKUU PROF. ELISANTE OLE GABRIEL ATEMBELEA KIWANDA CHA HUANRI MEDICAL GROUP BEIJING NCHINI CHINA
Mwambawahabari
Katibu
mkuu wa Wizara ya Viwanda ya Biashara na Uwekezaji, Prof Elisante
Ole Gabriel akiwa katika ziara ya kikazi nchini China (Beijing)
ametembelea kiwanda cha Huanri Medical Group kinachojishughilisha na
utengenezaji wa vifaa tiba, Mitungi ya Gesi na Matairi.
Akiwa
kiwandani hapo alishuhudia baadhi ya Vifaa vya tiba vinavyongenezwa
kiwandani hapo Fingertip/Handheld Oximeter ambacho hutumika kupima
kiwango cha hewa ya Oxygen katika damu (vinawafaa zaidi wakina mama
waja wazito na wazee), Anesthesia Machine inayotumika katika upasuaji
mkubwa pale ambapo mtu amewekewa dawa ya usingizi, Ventilator
inayotumika ICU kwa ajili ya kusaidia upumuaji kwa mgonjwa aliyezidiwa
pamoja na Kifaa kinachofahamika kama Health Machine (Mfano wa Briefcase)
kilichotengenezwa mahususi kwa ajili ya soko la bara la Afrika na
kinaweza kutibu takribani magonjwa 16 na kinabeba vifaa vingi ndani
yake.

Katibu
Mkuu wa Wizara ya Viwanda,Biashara na Uwezeshaji Prof. Elisante Ole
Gabriel akishiriki katika kuunganisha Mashine inayofahamika kama
"Anesthesia Machine" inayotumika katika usaidizi wa shughuli za
Upasuaji Mkubwa.

Katibu
Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwezeshaji Prof. Elisante Ole
Gabriel (Katikati) pamoja na ujumbe alioambatana nao, alipotembelea
kiwanda cha Huanri Medical Group jijini Beijing nchini China.
Akieleza
lengo la kutembelea kiwanda hicho Prof. Elisante alisema ni
kuzibaini fursa za uwekezaji zilizopo na jukumu la wizara ya Viwanda,
Biashara na Uwekezaji ni kuhakikisha kwamba wanajenga mazingira ya ya
wawekezaji kuwekeza vizuri bila kupoteza muelekeo na lengo kubwa la
kuinua Uchumi wetu. “tungependa tuwe na mikataba ambayo kwa vyovyote
vile hata kizazi kijacho kikija kuangalia hayo makubaliano kifurahi na
kuthamini kwamba waliongia katika makubaliano waliona mbele na
walijali maslahi mapana ya taifa.
Tunachoamini
ni kwamba wenzetu hawa wachina katika tasnia mbalimbali watakuja
Tanzania watawekeza, jukumu letu kubwa sisi na tunachokifanya ni
kuendelea kuwavutia kuwaweka katika mlengo ambao watafanya kazi zao
vizuri katika mazingira wezeshi na rafiki ili mwisho wa siku ajira
ziongezeke katika nchi yetu ya Tanzania lakini pia tuweze kuuza vifaa
vingi sana kutoka Tanzania kwenda kwenye masoko ya nje kwa ajili ya
kupata fedha za kigeni lakini lingine ambalo ni siri kubwa ya
mafanikio ni kupata pia utaalam ili vijana wa kitanzania waweze kupata
taaluma hii ambayo ni ya kiwango cha juu” Alisema Prof. Elisante.

akifanya mahojiano na vyombo vya habari baada ya kuhitimisha ziara yake kiwandani hapo

Akitazama moja ya hatua za kutengenezaji wa Vifaa vya Tiba kiwandani hapo

Katibu
Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Prof. Elisante Ole
Gabriel akisalimiana na Rais wa Kampuni ya Huanri Medical Group Bw. Wang
qianjun Mara baada ya kuwasili kiwandani hapo.

Katibu
Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Prof.Elisante Ole
Gabriel akizungumza jambo na Viongozi kutoka China - Asia Economic
Development Association Overseas Cooperation Committee, alioambatana nao
Kiwandani hapo.

Akionyesha furaha yake Katibu Mkuu alisema tayari Huanri Medical
Group wamekubali walau kwenye masuala ya taaluma ya vifaa tiba
wataweza kuwaalika vijana wetu wa kitanzania waje wakae China kwa
takribani miezi mitatu ili wapate utaalam wa kuunganisha vifaa hivi vya
tiba lakini lengo la serikali yetu ni kuona kiwanda hiki kikijengwe
Tanzania na hatua hii itapanua wigo wa ajira na pato la taifa litazidi
kuongezeka.
“
Huanri Medical Group ni miongoni mwa kundi kubwa la wawekezaji
wanaotarajia kuja Tanzania Mwezi Machi 2018 kwa ajili ya mikutano
mbalimbali ya uwekezaji na sisi tunawahakikishia kwamba serikali ya
awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dr. John Pombe Magufuli
inawakaribisha sana, na imani yetu ni kwamba Changamoto ya ajira itaweza
kupungua pale tutakapoendelea kuleta wawekezaji nchini.” Alisema Prof
Elisante.

Akihitimisha
ziara hiyo katika kiwanda hicho Prof. Elisante amewataka watanzania
kuendelea kupenda vitu vinavyozalishwa katika Taifa letu na kununua
vitu vyetu vya ndani. Amesema jambo la muhimu na kubwa ni upatikanaji
wa uhamisho wa technolojia kutoka China na kwamba tayari Tanzania
imeahidi kufanya kazi na wawekezaji hao kwa ushirikiano kwa lengo
la kuhakikisha ndoto na falsafa hii ya serikali ya awamu ya tano
inakamilika na kufikiwa kwa kwa kasi nzuri.”
Kwa
upande wake Rais wa kampuni hiyo ya Huanri Medical Group Bw. Wang
qianjun amefurahishwa na juhudi ambazo zinafanywa na Serikali ya
Tanzania kwenye sekta ya viwanda na ameahidi ushirikiano mkubwa na
kuonyesha utayari wake wa kuwekeza Tanzania .
Katika
ziara hiyo Katiba Mkuu wa Wizara ya Viwanda,Biashara na Uwekezaji
Prof. Elisante Ole Gabriel aliambatana na Afisa Mwandamizi wa Ubalozi wa
Tanzania nchini China Said Massoro, Viongozi kutoka China - Asia
Economic Development Association Overseas Cooperation Committee (Naibu
Katibu Mkuu Bi. Rui LU na Makamu wa Rais Bi. Tian Wenhui) Bw.Remidius
Emmanuel Katibu Mkuu wa Shirikisho la Wanafunzi Watanzania nchini
China pamoja Bi. Muka Kamuzora Mtanzania anayesoma Masuala ya Uchumi
hapa China.
mkuu wa Wizara ya Viwanda ya Biashara na Uwekezaji, Prof Elisante
Ole Gabriel akiwa katika ziara ya kikazi nchini China (Beijing)
ametembelea kiwanda cha Huanri Medical Group kinachojishughilisha na
utengenezaji wa vifaa tiba, Mitungi ya Gesi na Matairi.
Akiwa
kiwandani hapo alishuhudia baadhi ya Vifaa vya tiba vinavyongenezwa
kiwandani hapo Fingertip/Handheld Oximeter ambacho hutumika kupima
kiwango cha hewa ya Oxygen katika damu (vinawafaa zaidi wakina mama
waja wazito na wazee), Anesthesia Machine inayotumika katika upasuaji
mkubwa pale ambapo mtu amewekewa dawa ya usingizi, Ventilator
inayotumika ICU kwa ajili ya kusaidia upumuaji kwa mgonjwa aliyezidiwa
pamoja na Kifaa kinachofahamika kama Health Machine (Mfano wa Briefcase)
kilichotengenezwa mahususi kwa ajili ya soko la bara la Afrika na
kinaweza kutibu takribani magonjwa 16 na kinabeba vifaa vingi ndani
yake.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Viwanda,Biashara na Uwezeshaji Prof. Elisante Ole
Gabriel akishiriki katika kuunganisha Mashine inayofahamika kama
"Anesthesia Machine" inayotumika katika usaidizi wa shughuli za
Upasuaji Mkubwa.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwezeshaji Prof. Elisante Ole
Gabriel (Katikati) pamoja na ujumbe alioambatana nao, alipotembelea
kiwanda cha Huanri Medical Group jijini Beijing nchini China.
Akieleza
lengo la kutembelea kiwanda hicho Prof. Elisante alisema ni
kuzibaini fursa za uwekezaji zilizopo na jukumu la wizara ya Viwanda,
Biashara na Uwekezaji ni kuhakikisha kwamba wanajenga mazingira ya ya
wawekezaji kuwekeza vizuri bila kupoteza muelekeo na lengo kubwa la
kuinua Uchumi wetu. “tungependa tuwe na mikataba ambayo kwa vyovyote
vile hata kizazi kijacho kikija kuangalia hayo makubaliano kifurahi na
kuthamini kwamba waliongia katika makubaliano waliona mbele na
walijali maslahi mapana ya taifa.
Tunachoamini
ni kwamba wenzetu hawa wachina katika tasnia mbalimbali watakuja
Tanzania watawekeza, jukumu letu kubwa sisi na tunachokifanya ni
kuendelea kuwavutia kuwaweka katika mlengo ambao watafanya kazi zao
vizuri katika mazingira wezeshi na rafiki ili mwisho wa siku ajira
ziongezeke katika nchi yetu ya Tanzania lakini pia tuweze kuuza vifaa
vingi sana kutoka Tanzania kwenda kwenye masoko ya nje kwa ajili ya
kupata fedha za kigeni lakini lingine ambalo ni siri kubwa ya
mafanikio ni kupata pia utaalam ili vijana wa kitanzania waweze kupata
taaluma hii ambayo ni ya kiwango cha juu” Alisema Prof. Elisante.
akifanya mahojiano na vyombo vya habari baada ya kuhitimisha ziara yake kiwandani hapo
Akitazama moja ya hatua za kutengenezaji wa Vifaa vya Tiba kiwandani hapo
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Prof. Elisante Ole
Gabriel akisalimiana na Rais wa Kampuni ya Huanri Medical Group Bw. Wang
qianjun Mara baada ya kuwasili kiwandani hapo.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Prof.Elisante Ole
Gabriel akizungumza jambo na Viongozi kutoka China - Asia Economic
Development Association Overseas Cooperation Committee, alioambatana nao
Kiwandani hapo.
Akionyesha furaha yake Katibu Mkuu alisema tayari Huanri Medical
Group wamekubali walau kwenye masuala ya taaluma ya vifaa tiba
wataweza kuwaalika vijana wetu wa kitanzania waje wakae China kwa
takribani miezi mitatu ili wapate utaalam wa kuunganisha vifaa hivi vya
tiba lakini lengo la serikali yetu ni kuona kiwanda hiki kikijengwe
Tanzania na hatua hii itapanua wigo wa ajira na pato la taifa litazidi
kuongezeka.
“
Huanri Medical Group ni miongoni mwa kundi kubwa la wawekezaji
wanaotarajia kuja Tanzania Mwezi Machi 2018 kwa ajili ya mikutano
mbalimbali ya uwekezaji na sisi tunawahakikishia kwamba serikali ya
awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dr. John Pombe Magufuli
inawakaribisha sana, na imani yetu ni kwamba Changamoto ya ajira itaweza
kupungua pale tutakapoendelea kuleta wawekezaji nchini.” Alisema Prof
Elisante.
Akihitimisha
ziara hiyo katika kiwanda hicho Prof. Elisante amewataka watanzania
kuendelea kupenda vitu vinavyozalishwa katika Taifa letu na kununua
vitu vyetu vya ndani. Amesema jambo la muhimu na kubwa ni upatikanaji
wa uhamisho wa technolojia kutoka China na kwamba tayari Tanzania
imeahidi kufanya kazi na wawekezaji hao kwa ushirikiano kwa lengo
la kuhakikisha ndoto na falsafa hii ya serikali ya awamu ya tano
inakamilika na kufikiwa kwa kwa kasi nzuri.”
Kwa
upande wake Rais wa kampuni hiyo ya Huanri Medical Group Bw. Wang
qianjun amefurahishwa na juhudi ambazo zinafanywa na Serikali ya
Tanzania kwenye sekta ya viwanda na ameahidi ushirikiano mkubwa na
kuonyesha utayari wake wa kuwekeza Tanzania .
Katika
ziara hiyo Katiba Mkuu wa Wizara ya Viwanda,Biashara na Uwekezaji
Prof. Elisante Ole Gabriel aliambatana na Afisa Mwandamizi wa Ubalozi wa
Tanzania nchini China Said Massoro, Viongozi kutoka China - Asia
Economic Development Association Overseas Cooperation Committee (Naibu
Katibu Mkuu Bi. Rui LU na Makamu wa Rais Bi. Tian Wenhui) Bw.Remidius
Emmanuel Katibu Mkuu wa Shirikisho la Wanafunzi Watanzania nchini
China pamoja Bi. Muka Kamuzora Mtanzania anayesoma Masuala ya Uchumi
hapa China.
Hivyo makala KATIBU MKUU PROF. ELISANTE OLE GABRIEL ATEMBELEA KIWANDA CHA HUANRI MEDICAL GROUP BEIJING NCHINI CHINA
yaani makala yote KATIBU MKUU PROF. ELISANTE OLE GABRIEL ATEMBELEA KIWANDA CHA HUANRI MEDICAL GROUP BEIJING NCHINI CHINA Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala KATIBU MKUU PROF. ELISANTE OLE GABRIEL ATEMBELEA KIWANDA CHA HUANRI MEDICAL GROUP BEIJING NCHINI CHINA mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/11/katibu-mkuu-prof-elisante-ole-gabriel_28.html
0 Response to "KATIBU MKUU PROF. ELISANTE OLE GABRIEL ATEMBELEA KIWANDA CHA HUANRI MEDICAL GROUP BEIJING NCHINI CHINA"
Post a Comment