Sikio la Kufa....Chid Benz Adakwa Tena na Dawa za Kulevya...Polisi Msimbazi Wamshikilia..

Sikio la Kufa....Chid Benz Adakwa Tena na Dawa za Kulevya...Polisi Msimbazi Wamshikilia.. - Hallo rafiki WORLD MAELEZO LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Sikio la Kufa....Chid Benz Adakwa Tena na Dawa za Kulevya...Polisi Msimbazi Wamshikilia.., tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala biashara, makala general, makala hobby, makala karibuni info, makala michezo, makala siasa, makala utamaduni, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Sikio la Kufa....Chid Benz Adakwa Tena na Dawa za Kulevya...Polisi Msimbazi Wamshikilia..
kiungo : Sikio la Kufa....Chid Benz Adakwa Tena na Dawa za Kulevya...Polisi Msimbazi Wamshikilia..

soma pia


Sikio la Kufa....Chid Benz Adakwa Tena na Dawa za Kulevya...Polisi Msimbazi Wamshikilia..

Jeshi la polisi Mkoa wa Ilala, limewakamata watu saba akiwemo msanii wa muziki wa kizazi kipya, Rashid Makwiro maarufu kama ‘Chid Benz’ kwa tuhuma za kukutwa na dawa za kulevya aina ya Heroine.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Salum Hamduni amesema watuhumiwa hao walikamatwa Agosti 12 mwaka huu saa 11.50 jioni wakijihusisha na uuzaji wa dawa za kulevya.

Amesema jeshi la polisi limefanya msako wake na kuwakamata watuhumiwa hao wakiwa katika eneo ambalo linajihusisha na uuzaji wa dawa hizo.

 “Chid Benz na wenzake wapo kituo cha Polisi cha msimbazi ambapo tunaendelea na upelelezi ukikamilika tutawafikisha mahakamani na kiasi cha dawa zilizokamatwa zimepelekwa kwa mkemia mkuu na itajulikana ni kiasi gani za dawa za kulevya zilizokamatwa,”amesema Hamduni.

Hamduni amesema jeshi hilo linafanya msako liweze kubaini mtandao mzima unaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya na watumiaji ili kuhakikisha wote wanachukuliwa hatua na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Itakumbukwa kuwa , Oktoba 24,2014, Chid alikamatwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere(JNIA) jiji la Dar es Salaam akiwa na dawa za kulevya, akijaribu kuvuka nazo kwenda mkoani Mbeya kushiriki onyesho la Instagramu Party wakati akijua kuwa ni kinyume cha sheria .

Msanii huyo wa kizazi kipya alikiri shtaka hilo na ndipo , Februari 26 mwaka 2015, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ilipomhukumu kifungo cha miaka miwili jela au kulipa faini ya Sh900,000 baada ya kupatikana na hatia ya katika makosa matatu likiwemo la kukutwa na dawa za kulevya aina ya bangi na Heroine yenye thamani ya Sh 40,358.

Hata hivyo msanii huyo alifanikiwa kulipa faini na kukwepa kifungo hicho.


Hivyo makala Sikio la Kufa....Chid Benz Adakwa Tena na Dawa za Kulevya...Polisi Msimbazi Wamshikilia..

yaani makala yote Sikio la Kufa....Chid Benz Adakwa Tena na Dawa za Kulevya...Polisi Msimbazi Wamshikilia.. Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Sikio la Kufa....Chid Benz Adakwa Tena na Dawa za Kulevya...Polisi Msimbazi Wamshikilia.. mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/08/sikio-la-kufachid-benz-adakwa-tena-na.html

Subscribe to receive free email updates:

0 Response to "Sikio la Kufa....Chid Benz Adakwa Tena na Dawa za Kulevya...Polisi Msimbazi Wamshikilia.."

Post a Comment