title : BRAZUKA KIBENKI: Maofisa kuonyeshana kazi viwanjani
kiungo : BRAZUKA KIBENKI: Maofisa kuonyeshana kazi viwanjani
BRAZUKA KIBENKI: Maofisa kuonyeshana kazi viwanjani
MSIMU wa tatu wa michuano ya BRAZUKA KIBENKI unaoshirikisha taasisi za kibenki katika michezo ya mpira wa miguu na kikapu unatarajiwa kuanza mwishoni mwa mwezi huu jijini Dar es Salaam.
Katika msimu huu michuano hiyo itashirikisha timu 15 ambazo ni NMB (Mabingwa watetezi), DTB, Barclay’s, BancABC, Exim, Stanbic, BOA, UBA, Letshego, EcoBank, CRDB, BOT, Azania, TPB, Access na UBA.
Mmoja wa maofisa wa benki ya Exim, Frank Rweyemamu ambaye pia ni mwanachama wa tawi la Simba Makini linalomiliki mtandao huu alivitaja viwanja vitakavyotumika kuwa ni Gymkhana na DonBosco.
Martin Komba wa DTB (kulia) akimtoka Hezbo wa NMB katika pambano la jana
“Michuano ya mwaka huu itafanyika katika viwanja vya Gymkhana kwa mpira wa miguu huku mechi za mpira wa kikapu zikitarajiwa kuchezwa katika uwanja wa DonBosco.” Alisema Rweyemamu.
Jana kulikuwa na mchezo wa ngao ya hisani ambapo mabingwa watetezi NMB walikubali kichapo cha mabao 4-0 kutoka kwa DTB katika mchezo wa kuashiria kuanza kwa michuano hiyo.
Bingwa wa msimu huu atakabidhiwa kikombe pamoja na medali.
Hivyo makala BRAZUKA KIBENKI: Maofisa kuonyeshana kazi viwanjani
yaani makala yote BRAZUKA KIBENKI: Maofisa kuonyeshana kazi viwanjani Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala BRAZUKA KIBENKI: Maofisa kuonyeshana kazi viwanjani mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/07/brazuka-kibenki-maofisa-kuonyeshana.html
0 Response to "BRAZUKA KIBENKI: Maofisa kuonyeshana kazi viwanjani"
Post a Comment