Matukio : WASATU ilivyovimba Birmingham, Uingereza kusaidia Vigoli Bongo

Matukio : WASATU ilivyovimba Birmingham, Uingereza kusaidia Vigoli Bongo - Hallo rafiki WORLD MAELEZO LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Matukio : WASATU ilivyovimba Birmingham, Uingereza kusaidia Vigoli Bongo, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala biashara, makala general, makala hobby, makala karibuni info, makala michezo, makala siasa, makala utamaduni, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Matukio : WASATU ilivyovimba Birmingham, Uingereza kusaidia Vigoli Bongo
kiungo : Matukio : WASATU ilivyovimba Birmingham, Uingereza kusaidia Vigoli Bongo

soma pia


Matukio : WASATU ilivyovimba Birmingham, Uingereza kusaidia Vigoli Bongo






PICHA NA HABARI Za Freddy Macha


Jumuiya ya Wasanii Watanzania Uingereza (WASATU) ilichemsha supu, ukumbi wa Heartlands , Birmingham, Uingereza Jumamosi iliyopita. Makutano haya yalikuwa pia sehemu ya mchango mahususi kusaidia wasichana wanaopewa mimba kabla ya kuwa watu wazima, vijijini, Arusha. Fedha zilikusanywa na mjasiria mali mkazi wa Birmingham, Mtanzania Sia Travel.
Sia alijaa mlangoni akihakikisha kila senti iiliyolipwa na wahudhuriaji watashiba chakula , sanaa usiku kucha na kuwafariji vigoli wetu, Tengeru. WASATU iliyoundwa mwaka 2016 chini ya udhamini wa Balozi, Uingereza, Mhe Asha Rose Migiro, inakutanisha wasanii wa ala mbalimbali chini ya viongozi- mwanamuziki na mcheza sarakasi mwenye nidhamu ya hali yajuu, Fab Moses na mtangaza mapishi ya Kitanzania, Uingereza, Bi Neema Kitilya, aliyetulizana kama shingo ya twiga....Mwaka jana, 2017, shughuli hii ilifanywa Northampton na asilimia 20 ya kipato iliwafikia Watanzania waliofikwa na maafa ya mafuriko ya maji. Warembo wa kujitolea, walioonesha mavazi yaliyoandaliwa na kampuni ya “All Things African” (inayoendeshwa na Mtanzania, mchapa kazi, asiyejua uvivu kabila gani, Hamida Mbaga). Toka kushoto, Yvonne Waweru, Georgeous Katega, Victoire Koleilas, Maureen Tibenda Viongozi wa WASATU – Neema Kitilya na Fab Moses wakijadiliana huku shughuli zikikwea minazi, miguu na kuta. Fahari ya Tanzania – imesambazwa meza ya bidhaa mseto ya “All Things African” inayoendeshwa na Hamida Mbaga aliyesafiri toka Manchester. Mcheza ngoma aliyepitia mitihani mikali na vikundi maarufu vya mila zetu- Kibisa na Muungano - Likiwa Ismail- akionesha SINDIMBA – bila aibu, staha wala wasiwasi. Baadhi ya vyakula vya Kitanzania 7.
Rama Sax akipuliza vitu. Zamani alipiga na Simba Wanyika akashiriki kurekodi wimbo wa “Sina Makosa”. Rama Sax ni pia mwimbaji mahiri
Msanii wa mapishi Neema John aliyechangia kazi njema na Neema Kitilya. Wageni toka Tanzania na Uganda. Huyo Mganda (kushoto) ni mwanafunzi wa lugha ya Kiswahili Mpiga Gitaa mkuu wa shughuli, Jioni Ticha na kipande cha kuku baada ya jasho kali jukwaani. Alisafiri toka Leeds. Mbali si haba na hapa... Watanzania wakichangamkia tafrija ya msanii adilifu wa Kitanzania Sia Travel akihamasika. Mwanamuziki Saidi Kanda,(aliyesimama) mtukuzaji vyombo asilia vya muziki wa Kitanzania, akijumuika na Wabongo nadhif, waliokuwemo Mwandishi na mtunzi, Freddy Macha pamoja na Likiwa Ismail (ngoma) na Rama Sax.


Hivyo makala Matukio : WASATU ilivyovimba Birmingham, Uingereza kusaidia Vigoli Bongo

yaani makala yote Matukio : WASATU ilivyovimba Birmingham, Uingereza kusaidia Vigoli Bongo Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Matukio : WASATU ilivyovimba Birmingham, Uingereza kusaidia Vigoli Bongo mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/05/matukio-wasatu-ilivyovimba-birmingham.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "Matukio : WASATU ilivyovimba Birmingham, Uingereza kusaidia Vigoli Bongo"

Post a Comment