title : MPINA AAGIZA MKATABA WA OVENCO KUVUNJWA NA KUUNDWA KWA MKATABA MPYA.
kiungo : MPINA AAGIZA MKATABA WA OVENCO KUVUNJWA NA KUUNDWA KWA MKATABA MPYA.
MPINA AAGIZA MKATABA WA OVENCO KUVUNJWA NA KUUNDWA KWA MKATABA MPYA.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina ameagiza kuvunjwa kwa mkataba ulioundwa baina ya RANCHI ya Taifa NARCO na kampuni ya Overland kwa pamoja na kuunda kampuni ya OVENCO uliyokuwa na mapungufu ya kisheria na kiutendaji kufunjwa ifikapo mwisho wa mwezi huu wa December na kutoa mwezi mmoja kwa NARCO kuunda mkataba mpya wenye mwongozo wa kisheria.
Mpina aliyasema hayo jana alipokuwa katika ziara ya ukaguzi wa Ranchi ya Mzeri iliyopo wilayani Handeni Mkoani Tanga yenye ukubwa kwa Hekta 41,000 ambapo hekta 21,000 zinamililiwa na Muwekezaji kampuni ya Overland muwekezaji ambaye, amekuwa na mgogoro wa muda mrefu na NARCO ambapo baada ya Waziri Mpina kusililiza pande zote mbili na kujiridhisha na kumuona muwekezaji kutokuwa na uwezo wa kufikia malengo ya kuendeleza eneo lote la ardhi ambalo amekuwa akiliendeleza bila makubaliano yoyote ya kisheria, jambo ambalo limempelekea Waziri Mpina kuagiza NARCO kuingia katika hatua ya kuunda mkataba mpya baina yake na muwekezaji huyo utakaozingatia masharti mapya ya kisheria ikiwa ni pamoja na kuwepo kwa muwakilishi wa NARCO Katika kitalu hicho.
Aidha Waziri Mpina ameagiza muwekezaji huyo asihamishwe kwa kuwa ameonyesha nia ya kuendeleza eneo hilo kwa kuwepo kwa ng’ombe wambegu aina ya Borani pamoja na miundombinu mingine
Akizungumzia eneo la hekta 20,000 linalomilikiwa na wawekezaji wengine wadogo, Mpina aliwataka wawekezaji hao kulipa na kumaliza madeni yote ya kodi ya serikali wanayodaiwa katika vitalu vyao ifikapo January mosi 2018.
“Wawekezaji wengine wengine wanaomiliki vitalu katika ranchi hii ya Mzeri mnatakiwa kulipa madeni yote ya kodi mnayodaiwa na Serikali kodi mnayolipa ya shilingi elfu moja (1000) kwa mwaka ni kidogo sana lakini bado hamlipi, kinyume na hili ni bora muondoke wenyewe au tutawaondosha kwa nguvu muda huo ukifika. “ Alisisitiza Mpina.
“Baada ya kumaliza kulipa nawagiza NARCO kuwapa miezi mitatu wawekezaji hawa kuhakikisha wanaweka miondombinu inayolingana na ukubwa wa eneo na matumizi ya ardhi , tunataka wawekezaji wafikie malengo na mashamba haya yafanye kazi.” Alisema Mpina.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Handeni Godwin Gondwe alisema kuwa, Wiaya ya handeni itaendelea kulinda mazao na rasilimali za Mifugo kupitia sheria ndogondogo ambazo wilaya hiyo imejiwekea.
Akizungumza kwa namna ambavyo ameyapokea maagizo wa Waziri Mpina , mmiliki wa kampuni ya Overland Bw. Faisal Edha alisema kuwa amekubalina na maagizo ya Mpina na yupo tayari kuendelea na uwekezaji na anaamini kuwa mkataba mpya utanufaisha pande zote mbili.
Awali akipokea taarifa ya Mifugo ya wilaya ya Handeni, Waziri Mpina alimpongeza Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe. Godwin Gondwe kwa kuzitambua sheria za usimamizi wa mifugo na kuzitumia jambo ambalo litasaidia kwa kiasi kikubwa kutokuwepo kwa uonevu kwa watu wa jamii ya wafugaji na kuzitaka wilaya nyingine nchini kuiga mfano wa wilaya hiyo kwa kuunda sheria ndogo ndogo zitakazowaongoza katika sekta ya mifugo.
Ng’ombe aina ya Borani inayomilikwa na muwekezaji kampuni ya Overland katika Ranchi ya Mzeri , Wilayani Handeni Mkoani Tanga.
Katikati Waziri wa Mifugo na Uvuvi. Mhe. Luhaga Mpina akiongea vyombo vya habari baada ya ziara ya ukaguzi wa baadhi ya vitalu katika Ranchi ya Mzeri iyopo Wilayani Handeni Mkoani Tanga, kushoto kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Handeni Godwin Gondwe, na kulia ni mkurugenzi wa kampuni ya Overland Bw. Faizal Edha.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina kati kati na Mkuu wa Wilaya ya Handeni kulia Godwin Gondwe pamoja na wataalam kutoka Wizarani na Mkoani Tanga wakiwa katika zoezi la kukagua baadhi ya vitalu vilivyopo katika Ranchi ya Mzeri Wilayani Handeni.
Aliyesinama wa pili kulia ni Waziri wa Mifugo na uvuvi Luhana Mpina, kushoto kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Handeni Godwin Gondwe wakiangalia sehemu ya kunyweshea ng’ombe maji katika ranchi ya Mzeri wilayani Handeni.
Hivyo makala MPINA AAGIZA MKATABA WA OVENCO KUVUNJWA NA KUUNDWA KWA MKATABA MPYA.
yaani makala yote MPINA AAGIZA MKATABA WA OVENCO KUVUNJWA NA KUUNDWA KWA MKATABA MPYA. Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala MPINA AAGIZA MKATABA WA OVENCO KUVUNJWA NA KUUNDWA KWA MKATABA MPYA. mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/12/mpina-aagiza-mkataba-wa-ovenco-kuvunjwa.html
0 Response to "MPINA AAGIZA MKATABA WA OVENCO KUVUNJWA NA KUUNDWA KWA MKATABA MPYA."
Post a Comment