title : BREAKING NEWS: Yusuf Manji Atiwa Hatiani na Mahakama Kesi ya Kutumia Madawa ya Kulevya
kiungo : BREAKING NEWS: Yusuf Manji Atiwa Hatiani na Mahakama Kesi ya Kutumia Madawa ya Kulevya
BREAKING NEWS: Yusuf Manji Atiwa Hatiani na Mahakama Kesi ya Kutumia Madawa ya Kulevya
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu leo August 25, 2017 imemtia hatiani Mfanyabiashara Yusuf Manji katika kesi ya kutumia dawa za kulevya aina ya Heroin.
Uamuzi huo umetolewa na Hakimu Mkazi Mfawidhi Cyprian Mkeha, wakati kesi hiyo ilipoitishwa kwa ajili ya kutolewa uamuzi.
Hakimu Mkeha alisema kuwa ameridhika na ushahidi uliotolewa na mashahidi wa upande wa mashtaka na kwamba mshtakiwa ana haki ya kujitetea kutokana na mkojo wake kukutwa na dawa aina ya Morphine ambayo zao lake ni Heroin.
“Hivyo mshtakiwa anapaswa kujitetea kwa sababu Mahakama imemkuta na hatia,”
Baada ya kueleza hayo, Wakili wa utetezi Hudson Ndusyepo alidai kuwa mshtakiwa atajitete kwa hati ya kiapo ambapo watakuwa na mashaidi 15.
Hakimu Mkeha aliahirisha kesi hiyo hadi August 30 NA 31, 2017 ambapo itasikikizwa mfululizo.
Hivyo makala BREAKING NEWS: Yusuf Manji Atiwa Hatiani na Mahakama Kesi ya Kutumia Madawa ya Kulevya
yaani makala yote BREAKING NEWS: Yusuf Manji Atiwa Hatiani na Mahakama Kesi ya Kutumia Madawa ya Kulevya Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala BREAKING NEWS: Yusuf Manji Atiwa Hatiani na Mahakama Kesi ya Kutumia Madawa ya Kulevya mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/08/breaking-news-yusuf-manji-atiwa-hatiani.html
0 Response to "BREAKING NEWS: Yusuf Manji Atiwa Hatiani na Mahakama Kesi ya Kutumia Madawa ya Kulevya"
Post a Comment